Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia hoja iliyoko mezani. Uamuzi wa Serikali wa kuachia TBA kujenga majengo yote ya Serikali na Serikali za Mitaa ni uamuzi usiokuwa na tija. Haiwezekani TBA ifanye BOQ halafu ijenge yenyewe kitendo hiki ni kinyume kabisa na utawala bora na ni kinyume na sera ya Serikali ya PPP katika ujenzi wa majengo ya Serikali au Serikali za Mitaa. TBA ingefanya kazi yake ya manager wa miradi ya ujenzi kwa niaba ya Serikali kuhakikisha value formoney na ubora wa majengo.

Mheshimiwa Naibu Spika, TBA imezidiwa na miradi, wanashindwa kukamilisha miradi kwa muda na hata ubora wake kama ilivyotokea kwa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu. Ninashauri Serikali hili jambo litazamwe upya au kuhusisha sekta binafsi, sekta binafsi ndiyo engine of growth na ndivyo inavyotengeneza ajira kwa wingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uchukuzi, Serikali ina mradi mkubwa wa reli ya standard gauge. Mradi huo utawaajiri wataalam waliobobea katika nyanja mbalimbali. Katika wasilisho la Waziri wa Fedha na Mipango katika eneo la rasilimali watu idadi ya wanafunzi watakaopelekwa katika mafunzo kwa ajili ya mradi huu haijafahamishwa kinaga ubaga.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaishauri Serikali/Waziri mwenye dhamana ya uchukuzi awasiliane na Waziri wa Elimu ili kuhakikisha idadi inakuwa kubwa, ikionesha kwa namba ya wanafunzi watakaopelekwa vyuo vikuu pamoja na vyuo vya ufundi ili kutayarisha rasilimali watu ya kutosha kwa ajili ya reli ya standard gauge.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, Njombe kuna uwanja wa ndege ambao haujaendelezwa na upo karibu na makazi ya wananchi. Nahitaji majibu ya Serikali juu ya mipaka halisi ya uwanja wa ndege Njombe Mjini na nini hatua ya wananchi wenye makazi karibu na eneo la uwanja wa Njombe?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.