Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia kwa kuikumbusha, kuisisitiza Serikali kuhusu ujenzi wa barabara ya Ifakara – Mlimba – Taweta hadi Madeke Njombe. Barabara hii imeshafanyiwa upembuzi wa kina kuanzia Ifakara hadi Kihansi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ina umuhimu mkubwa kwa sababu inaunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Njombe. Vilevile Jimbo la Mlimba lina uzalishaji mkubwa wa mpunga, mahindi, ufuta, ndizi, cocoa na miti ya mbao (mitiki) ambapo yanapita magari makubwa ya tani 15 hadi 30 na kuifanya barabara hiyo ambayo ni ya vumbi na udongo chepechepe na ina mito mingi ambayo hutiririka mwaka mzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii inapita kwenye shamba kubwa la KPL la mwekezaji wa Kimarekani anayelima mpunga na mahindi kwa njia ya umwagiliaji na kufanya usafirishaji mazao kuwa mgumu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, umuhimu wa barabara hii ni kuokoa maisha ya wanawake wajawazito na watoto ambapo wanaposhindwa kujifungua huhitaji kukimbizwa Hospitali ya Rufaa St. Francis iliyopo Ifakara kwa sababu Wilaya au Jimbo la Mlimba hakuna hospitali ya uhakika na kwa hiyo husababisha vifo vingi vya wazazi. Hivyo tunaomba ijengwe kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa daraja la Kilombero limeshaanza kutumiwa na kwa kuwa kivuko kilichokuwa kinavusha abiria hakina kazi tena hapo darajani, hivyo basi Wilaya ya Kilombero tunaomba na tulikwisha omba kivuko hicho tukabidhiwe ili kikatumike kuvusha wananchi kwenye Jimbo la Mlimba eneo la Kikoi, Kata ya Utengule, Kijiji cha Ngalimala ambako Mto Kilombero unatenganisha Wilaya ya Kilombero na Wilaya ya Malinyi. Hii ni kwa sababu miaka yote wananchi wanatumia mitumbwi ambayo ni hatari na si salama kwa usalama wa wananchi hao.

Mheshimiwa Naibu Spika, mawasiliano katika baadhi ya kata na vijiji vya Jimbo la Mlimba yanapatikana kwa shida sana. Hivyo ni muhimu kusambaza huduma hiyo hasa kwa kuliwezesha Shirika la TTCL kwa kutumia Mkonga wa Taifa ili kuimarisha mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA ni muhimu ikawezeshwa ili itengeneze madaraja na barabara zinazounganisha kata na kata, kata na vijiji hata vitongoji ambazo zimeanzishwa na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mlimba lina mito mikubwa inayotenganisha kata na vijiji na kusababisha wananchi wengi kukosa huduma. Pia Kata ya Uchindile imetenganishwa kabisa na Makao Makuu ya Jimbo. Hivyo naomba muone umuhimu wa Jimbo la Mlimba kutengewa pesa za kutosha.