Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Wizara ya Uchukuzi kwa mafanikio makubwa katika sekta za ujenzi wa barabara ya Mtwara Corridor kutoka Mtwara – Mbinga; ufufuaji wa Shirika la Ndege la Tanzania; ufufuaji wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL); ujenzi wa reli ya Kati kwa kiwango cha SGR; na utendaji mzuri wa bandari zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi hiyo nzuri, naomba kuchukua fursa hii kueleza changamoto zinazolikabili Jimbo la Songea Mjini ambazo zinafanya utekelezaji wa Ilani ya CCM kuwa ngumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya mchepuko wa Mtwara Corridor -Songea Mjini (kilometa 11); ili Mtwara Corridor ikamilike ni lazima kipande cha mchepuko cha kilometa 11 kilichopo Songea Mjini katika Kata za Seedfarm, Msamala na Ruhumiko. Kutokukamilika kwa kipande hiki ambacho ni sehemu ya mradi namba 4197 ni kikwazo kikubwa sana katika mradi mzima wa Mtwara Corridor.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Songea Mjini hakuna hata barabara moja iliyotengewa fedha katika bajeti ya mwaka 2018/2019. Naomba sana barabara hii ya kilometa 11 ya mchepuko ya Mtwara Corridor - Songea Mjini ipewe kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Songea Mjini hakuna barabara hata moja katika bajeti nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba sana sana Mheshimiwa waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano barabara ya Mtwara Corridor - Songea bypass kilometa 11 iingizwe.