Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote natoa pongezi nyingi kwa Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa mengi ambayo yametekelezwa katika kipindi hiki kifupi cha uongozi wake akisaidiwa na Mheshimiwa Makamu wa Rais pamoja na Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana na Naibu Mawaziri wake wawili pamoja na watendaji wote wa Wizara hii kwa jinsi wanavyojitoa kuhakikisha sekta inafanya vizuri na kuleta tija kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe mapendekezo/maombi yafuatayo sambamba na mahitaji ya watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vyombo vingi kama siyo vyote vya usafiri (public transport) havina miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu hali inayopelekea wengi wao kushindwa kusafiri toka sehemu moja mpaka nyingine au kutumia gharama kubwa kwa kutumia usafiri wa kikundi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri/mapendekezo/ maombi kwa changamoto hii, kuwe na ukaguzi wa miudnombinu itayowezesha mtu mwenye ulemavu kupanda pasipo shida yoyote ama kuwe na ukaguzi maalum wakati wa uagizaji wa vyombo hivi nchini/miundombinu (uwepo wa miundombinu hii) iwe ni kigezo kimojawapo cha mtu anayetaka kufanya biashara ya usafirishaji kukidhi kabla ya kupewa leseni ya usafirishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto hii pia ipo kwenye usafiri wa treni zinazosafirisha abiria ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam. Watu wenye ulemavu wanashindwa kutumia usafiri huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu ni kwamba zinaweza kutengenezwa ngazi ambazo zitasaidia watu wenye ulemavu kuitumia anapohitaji kupanda. Vilevile nashauri kuwe na msisitizo wa sheria kwenye majengo mapya pamoja na miundombinu ya barabara mpya zinapojengwa vikidhi mahitaji ya watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, zinapotokea fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii katika Wizara hii, ni ombi langu kwamba kundi hili lifikiriwe. Fursa hizo ni pamoja na ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba upatikanaji wa habari na mawasiliano uwe rafiki kwa watu wenye ulemavu hasa wasioona na viziwi kwa kuzingatia matumizi ya lugha ya alama na maandishi ya nukta nundu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii na naomba kuwasilisha.