Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Wizara tajwa hapo juu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, uwanja wa ndege wa Kanda ya Kusini ulikuwa na taa kabla ya uhuru. Baada ya uhuru taa ziliondolewa na kupelekwa Arusha. Kutokana na mahitaji, sasa hivi Uwanja wa Mtwara ni uwanja wa Kanda lakini hauna taa. Ni lini kwenye bajeti hii taa zitawekwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais alisema akiwa Bukoba kuwa zimetengwa pesa shilingi bilioni 41 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mtwara. Mheshimiwa Waziri anasema shilingi bilioni 54 zimetengwa. Ni lini ukarabati utaanza? Kila mwaka yamekuwa yakisemwa haya na hamna utekelezaji, kwa nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna taarifa za chini chini kuwa ATC Bombardier wanataka kusitisha safari za Mtwara kwa kigezo kuwa abiria hawatoshi. Yapo mashirika binafsi mengi kwa mfano Precision Air wanaenda Mtwara kila siku asubuhi na wanapata abiria, iweje Shirika la umma lenye bei nafuu likose abiria?

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Kusini tunahitaji fursa ya Bombardier (ATC) tufaidi kama maeneo mengine. Naomba maelezo ya Mheshimiwa Waziri, kwa nini Bombardier inataka kuacha kuja Mtwara?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Wizara hii iweke minara ya simu kwenye maeneo ambayo haipatikani mitandao hasa maeneo ya mjini pembezoni mwa Mtwara na mtandao hakuna kabisa; maeneo hayo ni Mbawala Chini, Mkangala, Mkunjanguo, Naulongo na Dimbizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua ni lini maeneo haya ya Mtwara Mjini mtaweka minara ili mawasiliano yanapatikane?