Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini Shirika la Posta takribani miaka 10 sasa hawafungui masanduku mapya? Imeleta matatizo makubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, fidia ya bypass ya barabara ya Hangoni - Sigino kwa barabara ya Babati - Singida na Babati - Dodoma italipwa lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri TARURA wapewe 50% not 30%.

Mheshimiwa Naibu Spika, uwanja wa ndege Mkoa wa Manyara unajengwa lini? Eneo lipo Mamire Ngungu, Jimbo la Babati Vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halotel waliahidi kuweka mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Himit, Imbilili na Chemchem Jimboni kwangu. Jamani, hadi lini ahadi hii itatimia?

Mheshimiwa Naibu Spika, niwatakie kila la heri.