Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa kwanza nianze kwa kusema kwamba naunga mkono hoja. Lakini nina mambo machache ya kushauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza nilitaka nimuombe Mheshimiwa Waziri mwaka 2017 Septemba walitupatia fedha kwa ajili kufanya usanifu wa kilometa 149 barabara ya kutoka Tabora - Mambali - Bukene - Itobo kwenda Kahama. Lakini safari hii na mradi huu unaisha Desemba, 2018 huu nikuombe Mheshimiwa Waziri kwenye financial hiyo inayokuja kwa kuwa mtakuwa mmesha jua gharama mtutengee bajeti kwa ajili ya ujenzi ya ile barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo nataka niombe rehabilitation mmetenga fedha kwa ajili ya Mambali - Tabora na mmetenga fedha tena Mambali - Bukene hamjatenga fedha Itobo - Nzega kilometa 25 ninakuomba Mheshimiwa Waziri muiangalie hii kwa jicho la huruma sana ni muhimu sana msipofanya rehabilitation ile barabara itakatika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine ambalo nataka niseme Mheshimiwa Waziri sekta ya ujenzi inachangia almost asilimia kumi ya pato la Taifa la nchi yetu, na focus ya Serikali ni kufungua miundombinu. Nataka nikuombe Mheshimiwa Waziri leta mabadiliko ya sheria ya TANROADS ili tu-establish kitu kinaitwa preferential treatment kwa local contractors miradi mnayotenga fedha kwa ajili ya aidha, tumekopa ama fedha zetu za ndani angalau local contractors wapewe preference ili ile fedha iweze kubaki ndani ya uchumi wetu kwa kiwango kikubwa. Kwa sheria iliyoko sasa hivi inatoa preference only kama ni fedha za ndani, lakini hata fedha mnazokopa ni fedha za ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nilitaka niongee ni ukisoma hotuba ya Waziri ukurasa wa 170 mimi naunga mkono ujenzi wa standard gauge. Lakini Mheshimiwa Waziri ninachosikitika ni mabadiliko ya mwelekeo, ahadi yetu ya uchaguzi ilikuwa ni kujenga reli kutoka Dar es Salam na naomba ninukuu kidogo tu au kwa sababu ya muda niache ni kutoka Dar es Salaam kwenda Tabora, kwenda Mwanza; kutoka Tabora kwenda Kigoma, kutoka Uvinza kwenda Msongati; kutoka Kaliua kwenda Mpanda Kalemii. Kwenye kitabu chako cha bajeti mwaka huu tunakupitishia one point five trillion unatenga one point four kwa ajili ya phase one na two shilingi bilioni 100 unatenga kwa ajili ya kwenda Isaka kinachonishangaza hii decision basis ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa taarifa ya uchumi ya mwaka 2015/2016 mizigo kwenye bandari ilikuwa tani milioni tano asilimia 34 ni Zambia, asilimia 34 ni DRC, asilimia 12 ni Rwanda, asilimia sita ni Burundi our cash cow ni ku-save Eastern and Western Congo na Burundi kwa nini mnataka kumfanya Mnyarwanda kuwa hub wa Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Northen route inajengwa kwenda Rwanda na sisi tunampeleka line ya Isaka kwenda Kigali, kitakachotokea ataunganisha kwenda Msongati yeye ataihudumia Congo, ataihudumia Burundi na mkumbuke tuna East African Protocols ambazo zitamfanya yeye achague kutumia route anayotaka niwaombe kwa heshima tujenge reli yetu kutoka Makutupora Tabora, Tabora - Isaka, Isaka - Mwanza, Tabora - Kigoma, Uvinza - Msongati Kaliwa kwenda Kalemii, baada ya hapo tujenge kipande cha Isaka kwenda Rwanda tutakuwa tuna age over the others. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho tunajenga na reli bottom laini yake ni mzigo. Nataka nikuombe Mheshimwa Waziri tuanze preparation sisi bandari yetu ki-location na masoko tunayoyahudumiwa tuna-complete na Durban na Beira, nataka niwaombe naombeni mkaritafakari hili Mheshimiwa Waziri tuanzisheni, sasa hivi kwa regulation zetu za TRA mafuta ya transit yanakaa kwa siku 30, ni ya kwanza….

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.