Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii adhimu kabisa na mimi kupata kuchangia kwenye hoja iliyopo Mezani. Nitakuwa sijafanya sawa kama nisipomshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kunijalia uzima. Lakini si mimi peke yangu na Wabunge wenzangu tukakaa hapa tukajadili haya mambo ambayo ni mazuri kabisa kwa mustakabali wa maendeleo yetu na Taifa letu kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru mtoa hoja, Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake, Manaibu wake, kwa kazi kubwa, nzuri wanayofanya. Niwashukuru kwamba na sisi Dar es Salaam maeneo mengi tunaona kuna fedha zimetengwa, tunaamini zitaenda kuleta maendeleo kwa watu wetu wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu muda ni mchache na kama unavyojua watu wa Jimbo la Kinondoni wana mategemeo makubwa sana na bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya kuwaletea maendeleo na kuwaletea ili Kinondoni mpya tuliyokuwa tukiinadi kwenye kampeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, naanza na ujenzi wa nyumba kongwe za Magomeni. Nyumba hizi Mheshimiwa Rais alifanya uzinduzi pale akawaaminisha wananchi wangu wa Jimbo la Kinondoni, hasa wale waliokuwa wanakaa Magomeni, lakini vilevile na mimi nilitumia fursa ile kumuomba Mheshimiwa Rais nyumba hizi zikiisha watu wetu waliovunjiwa nyumba zao na wao wapate nafasi za kusihi, lakini nimeangalia kwenye kitabu cha bajeti hapa ukurasa wa 160 imeoneshwa kwamba kuna ujenzi unaendelea lakini nimeenda kutafuta pesa kule nimeona kuna shilingi milioni 200 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ninaomba Wizara walitazame hili kwa jicho la rehema kwa sababu watu hawa wana matumaini makubwa sana na ujenzi wa hizi nyumba na kwa sababu Mheshimiwa Rais alishatoa offer kwamba watu watakaa miaka mitano bila kulipa kodi, sasa tusipojenga kwa haraka inaweza ikafika hiyo miaka mitano hata Rais mwenyewe asiwawahi watu wake wakati wanakaa. Kwa hiyo, naiomba Wizara ituongezee fedha pale na ujenzi uishe kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi watu wa Dar es Salaam na hasa Kinondoni ambako mji ulikuwepo zamani tulikuwa na barabara nyingi nzuri za lami, hivi sana tuna barabara zetu zimechafuka sana, zina mashimo mengi. Lakini unaona kwamba tunatengewa mpaka barabara za changarawe na vumbi, pale Kinondoni utaweka wapi barabara ya vumbi? Ni barabara ambazo nyumba zimesongamana, unapoweka vumbi maana yake vumbi unawapelekea wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naomba sasa Waziri aangalie namna gani atazipandisha daraja barabara zetu za Manispaa ya Kinondoni. Mfano, tuna barabara muhimu sana, hii hapa ya Ndugumbi inakwenda pale Mwananyamala ya zamani sasa hivi inaitwa Makumbusho, Daraja la Harubu limevunjika, ile barabara tukiijenga tutasaidia watu kutoka katika njia kuu. Michepuko kwenye barabara inakubalika, labda kwenye mambo mengine huko ndiyo sina uhakika, lakini michepuko kwenye barabara ni jambo ambalo linasaidia sana kuondoa foleni.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa najikita, tuna barabara zetu za Tandale, kwa Bi. Mtumwa pale, tunahitaji ile barabara ipandishwe daraja ili ijengwe kwa kiwango kizuri. Tuna barabara zetu pale kwa Dunga, hii barabara ya Biafra ni barabara inatoka Biafra inakwenda kule Mwananyamala, ni barabara inayotumika sana. Lakini tuna barabara yetu nyingine inaitwa ya Biafra inayotoka pale kwenye mataa inakwenda mpaka Best Bite. Tuna barabara zetu za Kijitonyama - Akachube ni barabara ambayo Waheshimiwa Wabunge mtakumbuka bahati nzuri ni kwamba katika Jimbo langu la Kinondoni Wabunge wengi ni wakazi lakini vilevile hata wanaokaa nje wanapita pale. Kwa hiyo, barabara ile ya Akachube, barabara ya Mabatini ni barabara muhimu sana. Lakini Magomeni kuna matoleo, watu wa mwendo kasi pale Morocco pale karibu na Kanisa Katoliki ukitaka kuzunguka uje Manispaa au uende Chalinze…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, nakaa chini, ahsante.