Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili mimi niweze kuchangia Wizara ya Ujenzi. Kwanza kabisa nimpongeze Waziri, Naibu Mawaziri wote wawili, Katibu Mkuu wa Wizara na wataalam wote wa Wizara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja kwenye Mkoa wangu wa Tabora, nianze kuongelea suala zima la fidia. Kule Tabora tumepata pesa ya kujenga barabara ya Chaya - Nyahua ambayo ni barabara yetu kubwa tunayoitegemea kututoa Tabora mpaka Dar es Salaam na sehemu zingine lakini tunasumbuliwa sana na suala zima la fidia. Mkandarasi anapata shida sasa, anafanya kazi kipande hiki anaruka anaenda kufanya kazi kipande kingine anaruka. Uthamini ulishafanyika lakini bado fidia haijalipwa. Tunamwomba Mheshimiwa Waziri sana anapokuja hapa kujibu atupe commitment ya fidia hii italipwa lini. Vilevile kuna fidia ya Urambo - Kaliua bado haijalipwa, matokeo yake mkandarasi pia anasuasua lakini fedha zimeshapatikana bado fidia tu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna barabara ya Kaliua – Kazilambwa - Chagu ambayo ina kilometa 41 tu ili tutoke na lami kutoka Tabora mpaka Kigoma. Mheshimiwa Waziri, tunaomba mtupe pesa ya kilometa 41 ili tuweze kutoa hiki kipande kidogo sana kinachotuwekea doa. Kwa mfano, sasa hivi hii kilometa 41 haipitiki, kwa hiyo, lami yote mliyotuwekea inakosa maana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Tabora kuna barabara zimejengwa na TANROADS vizuri, lakini kuna tatizo la taa eneo la Isevya Tabora, usalama ni mdogo sana. Namuomba Mheshimiwa Waziri amuagize Meneja wa TANROADS wa Tabora atuwekee taa eneo lile kwa ajili ya usalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee barabara ya Ndala – Ziba, hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, tunaomba Mheshimiwa Waziri aiwekee lami.

Naomba niongelee reli ya kati ambayo sasa hivi inajengwa standard gauge, kule ambako standard gauge bado haijafika hali ni mbaya. Tunaomba itengenezwe wananchi wanakaa mpaka saa tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kuongea sasa maajabu ya miaka miwili na nusu ya Rais John Pombe Magufuli. Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli amejenga reli ya standard gauge kwa muda wa miaka miwili na nusu kitu ambacho huwezi ukakiamini. Ameanza Dar es Salaam- Morogoro na sasa hivi ameanza Morogoro-Makutopora, haijawahi kutokea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais amenunua ndege ambazo zinawatoa sana mapovu upande wa pili. Haya ni maajabu ya Rais John Pombe Magufuli ndani ya miaka miwili na nusu ameweza kutuletea ndege tatu na kwa taarifa yao kuna Boeing zingine ziko njiani zinakuja. Naonge haraka haraka siingii ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maajabu ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, flyover tumefika asilimia 72. Waambie waangalie ukurasa wa 22 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maajabu ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli, barabara line sita Morogoro Road, haijawahi kutokea Tanzania tukawa na highway …

T A A R I FA . . .

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, siwezi kujibishana na bwege, mimi siyo bwege. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kutaja maajabu ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika Wizara ya Ujenzi. Amenunua vivuko vinne: MV Kazi, MV Magogoni na MV Kivukoni kwa muda wa miaka miwili na nusu. Mimi najiuliza amewezaje ndani ya miaka miwili na nusu? Mbona sisi Wabunge kwenye majimbo yetu hatujaweza kufanya haya mengi kwa miaka miwili na nusu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naendelea na maajabu ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli; nawapongeza TCAA na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya ununuzi wa rada. Nawapongeza TPA, Mkurugenzi Kakoko anafanya kazi kubwa sana waongezewe tu kina cha bahari pamoja na pesa za ujenzi wa Gati Namba 7 mpaka 13 ili waweze kufanya mambo yao vizuri. (Makofi)

KUHUSU UTARATIBU . . .

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nilikuwa pia napenda kuiambia Serikali iwasaidie TTCL ili waweze kuendana na ushindani kwa kuhakikisha wanalipwa madeni wanayodai kwenye taasisi za Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maajabu mengine ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, ndani ya miaka miwili amepanua viwanja kadhaa vya ndege kikiwemo Kiwanja cha Tabora. Sisi tulikuwa tumekata tamaa, tulikuwa hatuna barabara ya lami tunayo, tulikuwa hatuna uwanja wa ndege upo, tulikuwa hatuna standard gauge inakuja, Mungu atupe nini, mambo ni fire. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi niwaambie tu ndugu zangu hawa wanaopenda kulalamika kila siku tusilalamike, tufanye kazi. Kila siku Serikali inaiba, inaiba haya mambo mazuri yamefanyikaje? Kama huu wizi unaotendeka kila siku na mambo haya mazuri yanafanyikaje? Wao ruzuku wanaiba hatusemi mpaka michango ya wagonjwa wameiba hatusemi. Wameenda kuomba msaada Ubalozi wa Ujerumani mgonjwa atibiwe wakati wametuchangisha humu mapesa, wamechangisha kwa mitandao, wamechangisha watu chungu mzima hela zote wameiba, sisi mbona hatusemi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba tu kuwaambia waache kusemasema sana, wafanye kazi ili Taifa liwe na maendeleo. Mbona Rais kila siku anaongea yeye ni Rais wa CHADEMA, wa CCM na wa Watanzania wote na analeta maendeleo ya Watanzania wote. Sijawahi kuona tukaambiwa madarasa yanajengwa kwenye majimbo ya CCM, majimbo ya upinzani hayajengewi madarasa, mimi sijawahi kuona lakini nashangaa ni kila siku shutumu Serikali inaiba, kushutumu Chato imejengewa kiwanja cha ndege. Jamani yule ni Rais wa nchi hii muwe mnaelewa, yule ni mamlaka hata vitabu vya dini vinatamka kutakuwa na mamlaka na ile ni mamlaka. Mkitaka msitake Mwenyezi Mungu ameiweka pale na itaendelea kuwepo pale mpaka muda wake utakapokwisha. Rudisheni hela za mgonjwa.