Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza kabisa nianze kwa kukushukuru kwa kunipa nafasi, lakini pia nitachangia dakika hizi tano specifically katika Mkoa wangu wa Singida, sitazungumzia masuala ya kitaifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumze kwa masikitiko makubwa sana, inaaminika na kwa uzoefu kwamba maeneo ambayo yanakuwa karibu na miji mikuu katika nchi mara nyingi huwa yananufaika kwa kiwango kikubwa sana na fursa ambazo zinakuwepo katika mji mkuu. Singida ni eneo ambalo liko pua na mdogo na mji mkuu wa Tanzania, lakini kuna mambo ambayo yanaonesha dhahiri shahiri kwamba Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi inashindwa kuwatendea haki wananchi wa Singida. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, treni ya kutoka Dodoma kwenda Singida imeshakufa toka mwaka 2009. Uchumi wa wananchi wa Singida kwa sehemu kubwa ni wafugaji, inaonesha kwamba kuna mifugo milioni moja na laki nne. Hawa wafugaji wanapotaka kutafuta masoko usafiri ambao ni bora na wa uhakika walikuwa wanatumia treni kwa ajili ya kusafirisha mifugo yao. Wakulima wa Singida walikuwa wanatumia usafiri wa treni kwa ajili ya kusafirisha mazao yao. Gharama za bidhaa kutoka maeneo mengine kuja Singida na kutoka Singida kwenda maeneo mengine zilikuwa za kiwango cha chini kwa sababu gharama za usafirishaji zilikuwa za kiwango cha chini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna ajira nyingi zimepotea kutokana na treni hii kutoonekana tena Singida pamoja na mama ntilie ambao walikuwa wanapika pale station, kulikuwa na vijana waliokuwa wanafanya biashara ndogo ndogo pale mpaka sasa hivi watu wale hawana uhakika wa maisha yao yanakwendaje. Nataka Waziri husika ajue kwamba wananchi wa Singida wanataka treni yao. Wananchi wa Singida tunataka treni yetu Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, airport ya Singida; huu ni mwaka wa 30 toka eneo kutengwa. Baada ya eneo kutengwa Naibu Spika nikikupeleka Singida sasa hivi huwezi kujua kama uko airport kwa sababu hata fence hakuna ni pori tupu liko pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, najiuliza and I want government kunijibu hapa, hivi mnapata hisia gani ambapo mnaona kwamba eneo ambalo mwaka 2010, mwaka 2015 wamekuwa champion kuwaweka kwenye viti hapa mnazunguka halafu leo ni mkoa ambao hata uki-google kwenye Wikipedia wanasema ni mkoa wa kimaskini Tanzania. Wananchi wa Singida siyo wajinga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, this is not fair. Wanakwenda kujenga International Airport Chato kwenye watu 365,000 mnaacha Singida ambako kuna watu 1,300,000. This is not fair at all, tumewakosea nini ninyi. Linapokuja suala la sikukuu ya Chama cha Mapinduzi miaka 30 ndio mnakuja mnatuletea ubwabwa, hatutaki ubwabwa tunataka maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, this is not fair, hii haikubaliki. Inaumiza sana karne hii eneo lenye hadhi ya mkoa ambalo lipo karibu na makao makuu ya nchi halina airport? Mambo mengine yote yamewashinda, hakuna hata chuo kikuu kimoja, hakuna treni, umeme wa upepo umewashinda, kila kitu kimewashinda Singida tumewakosea nini sisi? (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nafikiri niendelee tu na kuchangia kwa sababu nilipokuwa nazungumzia Chato sikusema Geita nimesema Chato kuna wananchi 365,000 asome ataona. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Iramba mpaka sasa hivi kwa muda…

T A A R I F A . . .

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei kwa sababu hata Singida kuna utalii vilevile.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Iramba kwa muda mrefu sana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)