Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai, hatimaye nimepata fursa hii kupitia wewe ya kuchangia hoja hii ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Niombe kuchukua fursa hii kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano, Rais wa hapa kazi tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Profesa Makame Mnyaa Mbarawa kwa kazi kubwa anayoifanya ikiwa ni pamoja na kunifundisha mimi siasa. Nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudie baadhi ya michango ambayo ni kuongezea au kukazia ambayo wamechangia wenzangu. Moja, ni kuhusu barabara inayounganisha Mikoa ya Morogoro na Ruvuma kupitia Wilaya yangu ya Namtumbo. Barabara hii tulitoa matumaini mwaka jana mwezi Julai kwamba imetoboka na kwa matumaini yale kuna watu wamepoteza maisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri nimemwandikia kilichotokea, naomba atusaidie kuikata zaidi ile barabara ili iweze kupitika, tuanze kupita kwa magari na pikipiki kabla hiyo lami haijaanza. Najua lami ni Ilani ya Uchaguzi ya Serikali ya Awamu ya Tano lakini vilevile ilikuwa Awamu ya Nne na tulianza usanifu Awamu ya Tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri, katika kipindi kifupi ameiwezesha barabara hii kukamilika kwa maana ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, umekamilika. Najua hii ni hatua kubwa sana katika ujenzi wa lami wa barabara hii. Nimwombe sana anisaidie kukikata kile kipande cha kuanzia Kilosa Kwampepo mpaka Londo ili tuweze kupita kutoka pande zote mbili; tukitoka Namtumbo kwa maana ya Kitanda, lakini vilevile tukitokea Kilosa, Kwampepo ambako sisi kule ndiyo nyumbani kwetu, kule ndiyo kuna mizimu yetu. Naomba sana atusaidie ili tuweze kufika katika maeneo ambayo ndiyo tunayaabudu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Profesa Makame Mnyaa Mbarawa kwa jinsi alivyonisaidia kukubali kuanza kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa kampeni. Ni kiongozi pekee aliyepita Barabara ya Mtwara - Pachani – Ligera – Lusewa – Magazini – Likusanguse hadi Nalasi wakati wa kampeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana kwa kutoa fursa hii ya kuanza kutekeleza ahadi hii kwa kumpata mkandarasi wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Namshukuru sana hii kazi inaendelea na naomba waendelee kutenga fedha ili Mhandisi Mshauri huyo aweze kuikamilisha hiyo kazi kwa wakati kwa maana ya mwakani, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Profesa Makame Mnyaa Mbarawa kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), ameuwezesha kwa namna ya ajabu kabisa kukamilisha mawasiliano kwa sehemu kubwa sana ya Wilaya ya Namtumbo. Nimwombe tu Mheshimiwa Waziri, akamilishe kipande hiki kidogo kilichobakia, tumebakiwa na kata kama tatu hivi ambazo hazina mawasiliano, mpaka leo bado wanalazimika kupanda kwenye miti au kusafiri umbali wa kilometa tatu, nne ili waweze kupata mawasiliano. Nimwombe Mheshimiwa Waziri anisaidie kupitia Mfuko huu wa Mawasiliano kwa Wote tukamilishe mawasiliano kwa Wilaya nzima ya Namtumbo kama ambavyo alianza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Waziri; kuna ahadi imetolewa na Taasisi yake ya TEMESA kutujengea kivuko. Sisi tunapakana na Msumbiji kwa maana ya Wilaya ya Namtumbo na tuna kivuko cha zamani sana, enzi na enzi, kinachotumika kufanya biashara kati ya Wilaya ya Mavago ya upande wa Msumbiji na Wilaya yetu ya Namtumbo. Nimwombe sana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.