Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Nianze tu kwa kuwashukuru na niseme tu kwamba Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, wanafanya vizuri. Nimefuatilia mambo mengi wanayoyafanya na nchi nyingi zinazofanya mambo ya barabara, wanafanya vizuri sana, tunatakiwa kuwashukuru sana. Tumpongeze Waziri Mbarawa, Katibu wake, Naibu Waziri na wote wanaohusika na Wizara hii kwa kweli wanafanya vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nianze tu na barabara za Mkoa wa Mara na niseme wakati fulani huwa najiuliza sijui kwa sababu mtangulizi wa Taifa hili alitoka Mkoa wa Mara na kwa sababu alikuwa anajumuisha Taifa hili kwa kuliona kama mtoto wa nyumbani kwake na akahusika kufanya maendeleo kwa kila eneo la nchi hii, lakini sasa Mkoa wa Mara kwa maeneo mengi hayaendi vizuri kwa kweli. Ukitazama barabara zetu barabara ya Nyamswa - Bunda tumeahidiwa toka mwaka juzi na iliwekewa shilingi bilioni nane mpaka leo iko kwenye utafiti tu hakuna kinachoendelea hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Buramba inatengenezwa haiendi, barabra ya Makutano - Sanzati haiendi, barabara ya Sanzati - Makutano - Mugumu haiendi, reli ya Arusha - Tanga - Musoma haiendi na Uwanja wa Ndege Musoma hauendi. Kwa hiyo, tunaomba kwa kweli Mheshimiwa Waziri uutakapokuja hapa uje na majibu kamili kwamba hizi barabara tulizozitaja hapa zinakwenda vizuri na unaandaa namna gani unaweza kusaidia vinginevyo tunaweza kung’anga’ania shilingi yako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mawasiliano, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuzungumzia masuala ya mawasiliano, niliomba kata tano, kwa maaa ya mawasiliano, nimepata kata moja kwa mtandao wa Halotel. Kuna vijiji vya Nyangere, Tingirima, Nyabuzume, Marambeka, Nyagurundu vyote havina mawasiliano. Kwa hiyo, nafikiri ni vizuri mnapokuja hapa muone ni namna gani ya kutusaidia, na ndugu yangu Nditiye uko hapo nadhani utanisaidia katika suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tu kwa kusema mambo mengine madogo madogo haya lakini ni makubwa kwangu, nashangaa kuona vitu vingi vinazungumzwa hapa, sijui kuna shilingi trilioni 1.5, kuna ngapi, lakini sisi ambao tumeingia humu bado ni wageni kwenye Bunge hili tunajua utaratibu wa CAG unafuata kanuni ya kwenda kwenye Kamati ya PAC ambayo ndiyo inaita watu wote wanaohusika na ile mijadala kule ndani na kuona kile kinachohusika na kama uthibitisho utakuwa haupo ndipo tunajua kwamba hizi hela zimepotea au hazijapotea. Sasa naona watu hapa mishipa imewatoka, trilioni zimepotea, wapi sasa? Nani amekwenda kuthibitisha kwamba hela zimepotea? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika report ya CAG tumeona mengi, tumeona kuna vyama hapa vimepoteza hela nyingi, tumeona kuna vyama vingine vimeshindwa kupeleka hela hatusemi wameiba, tunasema ni vitu vimo ndani, kwa nini watu wameshupaa? Lakini mbaya zaidi inaonekana ni kama kwamba hizi hela ni kama vile zimechukuliwa na Rais wakati Rais si mtu wa masuhuli sasa ni maneno gani haya? Yaani kuna vitu vingine vinanga’ang’aniwa kiasi kwamba wakati mwingine huwezi kujua kama vina maana gani hivi. Jamani katika mtu ambae atakuwa wa mwisho kuhukumiwa katika Taifa hili kwamba ni mdhulumati, kwamba ni mwizi, kwamba ni mtu anayekula rushwa ni Rais John Pombe Magufuli, wananchi wanamjua ndiye namba moja kwa uaminifu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.