Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza kabisa naomba nianze kwa kuishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi kubwa inayofanywa ya kuendeleza miundombinu ikiwemo ya barabara. Naomba nitoe shukrani zangu kwa kuwa tumeona Arusha inazidi kukua, tumeona barabara ya Tengeru mpaka Sakina kilometa 15, tumeona by-pass ndani ya Jiji la Arusha ambayo inaendelea kupunguza msongamano katika jiji la Arusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa kuliko yote naomba niishukuru Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa barabara ya Ngorongoro. Tumeona barabara ya lami ya kilometa 50 inayofika mpaka Waso ambayo ni kiwango cha lami. Barabara hii itawasaidia sana akina mama wa Arusha katika kufanya biashara zao hasa Ngorongoro kwa ajili kusafirisha bidhaa zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende moja kwa moja katika masuala ya anga. Tumekuwa tukidhiakiwa na kupata aibu kuambiwa tunazidiwa na nchi ndogo kwa ajili ya ndege, lakini tumeona kazi aliyoifanya aliyofanya Mheshimiwa Rais kwa kutuletea ndege. Tumeona upande wa pili walikuwa wanasema shirika limekufa, likafufuliwa, tumeletewa ndege wakawa wanasema ndege hazijaja, sasa hivi ndege zimekuja wameingia wanansema kuna ufisadi katika manunuzi, jamani hivi hawa watu wanataka nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunamwambia Mheshimiwa Rais wetu afanye kazi kwa sababu kelele za chura hazimzuii ng’ombe kunywa maji. Vilevile tunajua kabisa mwanaume wa kisukuma amewashika pabaya, na bado, itakapofika mwaka 2020 wataendelea kulialia kwa Watanzania na ndipo Watanzania watakapoamua, kwamba watafuata machozi au watamrudisha mwanaume wa Kisukuma? Amewashika pabaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba moja kwa moja nielekeze mchango wangu katika Uwanja wa Ndege wa Arusha. Bajeti iliyopita walisema watakarabati Uwanja wa Ndege wa Arusha kwa kuongeza sehemu ya kugeuzia ndege na ya kurukia, lakini mpaka sasa hivi bado haujaongezwa; tumesahau kuwa Arusha ni Jiji la kitalii na watalii wengi wanatumia ndege zetu kwa ajili ya kuingia na kutokea Arusha. Kwa hiyo tumekuwa tukikosa mapato mengi kutokana na watalii wetu ambao wanaanzia Dar es Salaam au wanaanzia KIA, watalii ambao wanakwenda Kanda ya Kaskazini ikiwemo na Arusha.

Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana Mheshimiwa Waziri aniambie kwa sababu mwaka wa jana kulikuwa na uwanja wa Ndege wa Arusha lakini sasa hivi sijaona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba moja kwa moja nijielekeze kwenye……

T A A R I F A . . .

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza taarifa yake siitaki, anaelewa kabisa mwanaume wa Kisukuma anayewasumbua ni Rais John Pombe Magufuli, sina haja ya kumwambia, anatafuta kiki, Magufuli anawasumbua sana na bado kwa kazi kubwa anayofanya ya kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi. Tunajua hamlali kwa ajili yake, mnamchafua halafu mnakuja kumuomba barabara, hebu tulieni huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijielekeze kwenye Shirika la Posta ambalo limekuwa likiwalipa waliokuwa wafanyakazi wa Jumuiya ya Posta ya Afrika Mashariki ambao wanalipwa kwa niaba ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tunaomba Serikali iwalipe zile pesa ambazo walikuwa wanawalipa Shirika la Posta, shilingi bilioni nne wawalipe ili na wenyewe waendelee kujiendesha vizuri.

Tumeona reli ya standard gauge inakuja, ambayo itatusaidi sana wamekuwa wakiikashifu lakini hiyo italeta maendeleo kwa wananchi na hatimaye wananchi wanatuuliza maendeleo. Tunajua, tunaposema mwanaume wa kisukuma linawauma sana kwa sababu mwanaume wa kisukuma ambaye ni kiongozi wetu Tanzania nzima ni mmoja na anafanyakazi na ni Rais wetu John Pombe Magufuli, anatekeleza Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi, anaendelea kuleta maendeleo na Watanzania wote wanajua hata…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)