Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa sababu ni mara yangu ya kwanza kuchangia, naomba kwanza kuanza kwa kutoa shukurani. Moja kwa Mwenyezi Mungu; pili, kwa wazazi wangu; baba yangu na mama yangu, kwa kunilea, kunisomesha na zaidi ya yote kwa kunipa ujasiri mpaka nimeweza kufika hapa leo. Baba na mama nawashukuruni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nachukua fursa hii kuwashukuru akinamama wote wa Mkoa wa Iringa kwa kunidhamini, kwa kuniamini niwe mwakilishi wao. Kweli mmenipa heshima kubwa sana. Naomba mwendelee kuniombea Mwenyezi Mungu anipe nguvu, hekima na busara ili tuweze kushirikiana vyema tuisaidie Iringa yetu iweze kusonga mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, pia nitoe pongezi zangu kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kazi kubwa na ngumu anayoifanya kwa kujitoa muhanga, awe kimbilio, awe macho ya maskini na wanyonge. Mheshimiwa Rais, nakushukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwa niaba ya wanawake wote wa Mkoa wa Iringa, namshukuru tena Mheshimiwa Rais kwa kumchagua Mama yetu Samia, kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hii inadhihirisha anatutambua sisi wanawake, anatambua mchango wetu kwa nchi hii na anataka tuendelee kushiriki kikamilifu katika maamuzi yatakayohusu Serikali ya nchi yetu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais tunakushukuru sana. Mama Samia hongera sana; najua utatuwakilisha vyema na sisi wanawake wa Tanzania tupo nyuma yako. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba niende moja kwa moja, niunge mkono hoja iliyoletwa mbele yetu na Wizara ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji. Natambua kuwa Serikali yetu inajipanga kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya viwanda ili tuweze kupambana na hili tatizo sugu la ajira na umaskini hasa kwa vijana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua kuwa asilimia 75 ya Watanzania, wanategemea aidha kilimo, uvuvi na ufugaji. Sasa wakati Mpango wa Maendeleo umeletwa hapa kujadiliwa, wengi tulishauri kuwa corner stone ya huu uchumi wa viwanda, viwe vikubwa au vidogo lazima vitumie raw materials ambazo zitakuwa zinazalishwa na hawa wakulima wadogo wadogo ambao wanatoka vijjini. Lengo lilikuwa, kusaidia kupata soko na ku-add value ya hizi hizi raw materials ambazo zitakuwa zinazalishwa na hawa wakulima wadogo wadogo. Kwa kufanya hivyo, tutasaidia kuinua uchumi wa wakulima na kuisaidia Tanzania iweze kufika kwenye huu uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi kama Malaysia na India, zilikuwa nchi maskini. For example Malaysia was one of the poorest country kuliko hata Tanzania, lakini wenzetu wameweza kupiga hatua na sekta ambayo imeweza kuwafikisha hapo ni Sekta ya Kilimo. Waliwatengenezea mazingira mazuri wakulima hawa wadogo na wafugaji wadogo wadogo. One of the things they did ni kutengeneza hizi collection centers; zikawa ni kiunganaishi kati ya wafugaji, wakulima na viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hizi collection centres zinasaidia huyu mfugaji au mkulima anapoamka asubuhi wazo lake kubwa ni kuzalisha na siyo soko la mazao yake; lakini hapa Tanzania bado kidogo tuko nyuma. Kwa mfano, mifugo; Tanzania is one of the leading countries kwenye mifugo, lakini bado tuna-import maziwa kutoka nchi nyingine. What is problem here? Hatuna viunganishi, hatuna collection centers ambazo zitawaunganisha hawa wafugaji na viwanda vilivyopo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitatoa mfano kidogo tu. Pale Mkoani kwangu Iringa tuna kiwanda kikubwa cha Asasi, kina-process products nyingi zinazotokana na maziwa; mengine tunatumia hapa kwenye restaurant yetu ya Bunge, naomba mwendelee kutuunga mkono. Kiwanda hiki kinaweza ku-process lita 100,000 kwa siku, lakini mpaka leo hii kinapokea maziwa lita 15,000; na hizi zitoke Mikoa mitatu; pale Iringa, Njombe na Tanga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, cha kusikitisha zaidi, pale Iringa kuna wafugaji ambao maziwa yanaozea ndani. Tatizo hapa ni nini? Ni kile ambacho nimesema kwamba hatuna viunganishi, hatuna collection centers ambazo zitawaunganisha hawa wafugaji na hiki kiwanda kilichoko pale. Kwa hiyo, Waziri Mheshimiwa Mwigulu nakuomba, umefanya kazi kubwa kwenye Mkoa wangu wa Iringa, naomba ufike pale tuwe kiunganishi, tuwatengenezee hizi collection centers kwenye Wilaya yangu ya Mufindi, Wilaya ya Iringa Mjini, Iringa Vijijini na Kilolo. This will be a win-win situation. Tutakuwa tume-create soko kwa wale wafugaji wadogo wadogo na pia tutam-assure raw material huyu mwekezaji ambaye amefungua kiwanda pale Mkoa wa Iringa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine ambacho ningependa kushauri, tu-invest kwenye elimu. Wakati TAMISEMI wanawasilisha bajeti yao, ilionesha kuwa kuna hawa Maafisa Ugani, less than fourteen thousand, kuna thirteen thousand five hundred and thirty two. Hii ni namba ndogo and this can be easily solved.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna watoto wengi ambao wamemaliza Shule za Kata, tuwape incentives. Hizi ruzuku tunazotoa kwenye pembejeo, tuhakikishe tunawekeza kwenye elimu. Hawa Maafisa Ugani ndiyo watakaokuja kuwa Walimu wa kuwafundisha huyu bibi na babu kwa sababu lengo ni kuhakikisha hii asilimia 75 inaendana na huu uchumi wa viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimpongeze Waziri wa fedha kwa kutambua unyeti wa Sekta hii ya Kilimo akaahidi kutoa nyongeza ili iweze kutusaidia kufikia malengo ya uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba nihitimishe kwa kusema yafuatayo:-
Tanzania ya viwanda inawezekana, Tanzania ya uchumi wa kati inawezekana; uzuri Sekta hii imepewa Waziri Mheshimiwa Mwigulu aliye makini, ambaye yuko competent, ambaye atatufikisha pale tunapotaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi.
MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.