Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naunga mkono hoja. Naipongeza Serikali ya CCM katika juhudi za makusudi za kuwasaidia wananchi hasa wanawake na watoto kupata afya bora na huduma nyinginezo za kijamii. Naishukuru na kuipongeza Serikali kwa hatua iliyochukua kuanzisha matibabu ya kupandikiza figo na upasuaji wa moyo hapa nchini. Pia naipongeza Serikali kwa kuanzisha chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri, naiomba Serikalii iangalie namna ya kupunguza bei ya vifaa vya kujifungulia kwa mama wajawazito ili akina mama wasio na uwezo waweze kumudu gharama za vifaa hivyo. Serikali ijenge vituo vya kuwasaidia vijana walioathirika na madawa ya kulevya na bangi ili warudi katika hali yao ya kawaida na waungane na wananchi wenzao katika ujenzi wa Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mayoma kwa akina mama yanazidi kuwa tatizo kwa wanawake ni vyema ufanyike utafiti juu ya ukubwa wa tatizo hilo na baadae elimu itolewe kwa wanawake waende hospitali kabla ya matatizo hayajawa makubwa na kusababisha madhara mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naipongeza Wizara na viongozi wote wa Wizara kwa juhudi kubwa wanazofanya katika kuisimamia Wizara na utekelezaji wa majukumu yote kwa bidii, waendelee na moyo huo. Pamoja na Madaktari Bingwa akiwepo Dkt. Janabi, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii.