Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kutoa pongezi za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Tano na Wizara ya Afya kwa kazi nzuri ya kuboresha huduma za afya. Pamoja na changamoto hizo, napenda kutoa maoni yangu kuhusu changamoto zifuatazo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Kituo cha Afya Mjimwema - Songea Mjini; kituo hiki cha afya kinafanya kazi kama Hospitali ya Wilaya, hivyo basi kufanya kazi kubwa kuliko uwezo wake. Kituo hiki cha afya kinakabiliwa na changamoto zifuatazo; ukosefu wa wodi ya wanawake na wanaume, ukosefu wa x-ray, MRI na vifaa tiba vingine, ukosefu wa gari la wagonjwa (ambulance) na uchakavu wa majengo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Songea una jumla ya wakazi 230,000 lakini hakuna Hospitali ya Wilaya. Tunahitaji Hospitali ya Wilaya ili kuhudumia wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vituo vya afya; Wilaya ya Songea Mjini yenye jumla ya wakazi 230,000 na kata 21 haina Hospitali ya Wilaya. Tunahitaji vituo vya afya angalau vitatu katika Kata za Ruvuma, Ndilima Litembo na Mletele.