Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia kuwa wazima wa afya zetu na tunaendelea na harakati zetu vizuri. Pia ninapenda nitoe shukrani zangu za dhati kabisa kwako wewe kwa namna unavyosimamia Bunge hili kwa umakini na umahiri mkubwa kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nichangie Wizara hii ya Afya kwa mambo yafuatayo; malaria, UKIMWI, maradhi ya figo na maradhi yasiyo ya kuambukiza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba malaria yameshuka nchini kwa kiasi cha afadhali, lakini kwa namna Serikali ilivyojisahau uwezekano wa kurudi tena kwa kasi upo. Hivyo basi ni vyema Serikali ikafikiria tena namna ya kupambana na malaria. Ni vyema Watanzania wakawekwa mbali na malaria.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Taifa linaelewa sana jinsi athari za UKIMWI zinavyoweza kupunguza nguvukazi ya Taifa, ni vyema Serikali ingeongeza juhudi zaidi katika kuwaelimisha watu wetu. Lakini pia hizi dawa za ARV ni vyema ikawa ni rahisi zaidi kupatikana katika kila eneo la nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa nitoe pongezi kwa Wizara kuhusiana na kadhia hii, Taifa limeweza kulipa fedha nyingi sana kwa kuwatibu watu wetu nchini. Kwa namna ya pekee, ninapenda niishauri Serikali iendelee kufunza zaidi wataalam wa fani hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ya pekee naomba niishauri Serikali kutoa taaluma ya kutosha kuhusiana na vipi Watanzania wataweza kujilinda na maradhi haya, yakiwemo pressure, sukari na kadhalika. Kwa kasi ya kutisha maradhi haya yanajitokeza kwa watu wetu na pia namna ya kuwatibu haijakuwa maridhawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala hili la vifaatiba, bado kabisa Taifa letu lina tatizo kubwa sana. Ukienda hospitali zote za rufaa utawakuta wagonjwa wengi wamepanga mistari wakiwa wanasubiri kupata huduma za x-rays, CT-scan, ultra sound na vifaa vingine. Mimi ninadhani huu sasa ndiyo wakati wa kuacha porojo na kufanya kazi kubwa ya kujenga afya zetu kwa kuvitafuta vifaa hivi na kuvieneza katika hospitali zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu usambazaji wa dawa; hapa napo pana uzembe mkubwa. Hivi inakuwaje Serikali inanunua au inatengeneza dawa kwa maslahi ya Watanzania wakati wa kuzisambaza dawa hizi eti kuna maeneo hazifiki, zinapelekwa wapi na nani? Ninaomba hapa Waziri atakapofanya majumuisho atoe majibu ya swali hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na utumishi wa Wizara, ni ukweli usiofichika kwamba Wizara hii ina uhaba mkubwa wa watumishi, yawezekana ndiyo maana utendaji wa Wizara hii unasuasua, siyo mzuri, malalamiko ni mengi, wagonjwa wanarundikana mahospitalini, watabibu ni haba. Ni vyema Serikali ikafikiria vizuri na ikaajiri vijana kwa lengo la kuziba hii mianya.

Mheshimiwa Naibu Spika, uhaba wa hospitali; bado kabisa hospitali ni haba sana kulingana na ukubwa wa nchi yetu. Tanzania ya sasa inahitaji hospitali kama za Muhimbili angalau 10 katika Mikoa yote mikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.