Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kujenga hospitali ya kisasa ya Benjamin Mkapa iliyopo Dodoma, lakini napenda kuishauri Serikali kwamba hospitali ile ina upungufu mkubwa wa madaktari pamoja na wauguzi. Hivyo basi Serikali iangalie hospitali ile kwa ukaribu mkubwa kwani inahudumia wananchi wa maeneo mengi sana kama vile UDOM ambapo wanafunzi takribani wote wanatibiwa pale, Wabunge na wananchi wa Dodoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na ongezeko kubwa la udhalilishaji wa wanawake na watoto. Naishauri Serikali iweze kutoa mafunzo pale akina mama wanapokuja kliniki ni namna gani inapotokea kubakwa kwa mtoto wake. Katika hatua ya awali kitu gani afanye ili ushahidi wa awali uweze kupatikana. Mara nyingi ushahidi huu hukosekana kwa vile huwasafisha kwa kuwakosha wakiona wanaweka vizuri kumbe wanapoteza ushahidi.