Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Wizara ya Afya namshukuru sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kufanya ziara katika jimbo langu na kujionea changamoto.

Nashukuru kwa kupewa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Kirando na kuokoa vifo vya hasa akina mama. Pia nashukuru sana kwa kupewa pesa mwaka huu kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Nkasi kwa kuwa tuna miaka 40 hatuna Hospitali ya Wilaya, shukrani sana kwa Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tuna vituo vya afya viwili tu, naomba kujengewa kituo cha afya katika Kata ya Kabwe na Korongwe maana kata hizo ziko mbali na Makao Makuu ya Wilaya na wakazi ni wengi, pia usafiri ni mbaya sana na hata hivyo, nilipeleka gari la wagonjwa
nililopewa na Rais wetu ili lisaidie katika kata hizo mbili, hilo gari limekuwa ukombozi mkubwa sana tena sana, ni ukombozi sana kwa wagonjwa wa kata hizo mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana tena sana Mheshimiwa Rais Magufuli kwa msaada na ukombozi kwa hilo gari. Pia shukurani sana kwa Waziri Ummy Mwalimu na Naibu Waziri Dkt. Ndugulile kwa jitihada zao.