Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na pongezi kwa Wizara inafanya mageuzi makubwa katika sekta na hivyo kuboresha huduma za afya kwa upana wake. Hongera kwa timu nzima ya Wizara ikiongozwa na Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu na wataalam wote na wasaidizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Tunduru na Jimbo la Tunduru Kaskazini, katika Hospitali ya Wilaya chumba cha upasuaji tunaomba replacement na improvement ya vifaa hususan operation beds/tables ikiwa ni pamoja na ukarabati wa chumba chenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uhaba wa wataalam, nafahamu changamoto hii iko karibu katika maeneo yote nchini, naomba Wilaya ya Tunduru itazamwe kama eneo la pembezoni na lililosahaulika kwa miaka mingi (disadvantaged). Tunaomba apatikane DMO kwani aliyepo anakaimu nafasi hiyo. Pia kuna uhaba mkubwa katika vituo vya afya na zahanati hususan Kituo cha Afya cha Matemanga na Nakapanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Matemanga kilitengewa fedha kiasi cha shilingi milioni 500 kwa madhumuni ya ukarabati na uboreshaji wa vifaa. Fedha hizo hatujaletewa hadi leo na taarifa za awali nilizonazo, fedha hizo zimepelekwa eneo lingine. Sio muhimu sana kupata/kujua sababu ya kuwa diverted fedha hizo, lakini ninaomba tupatiwe fedha kama ilivyopangwa awali.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna mahitaji ya gari la wagonjwa; nimesikiliza hotuba iliyosomwa na Mheshimiwa Waziri wa Afya, hongera kwa kutenga fedha kwa ajili ya magari ya wagonjwa (ambulance) 17. Ombi langu ni kupewa angalau gari moja kwa Tunduru Kaskazini ambako Hospitali ya Wilaya iko. Izingatiwe pia kwamba (location) mahali Hospitali ya Wilaya ilipo inasababisha baadhi ya wanaohitaji huduma za rufaa kutoka katika zahanati wanatoka umbali wa kufikia hadi kilometa takribani 100.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Kituo cha Afya Nakapanya, tumekamilisha ujenzi wa jengo la upasuaji katika kituo hiki. Ombi ni kupatiwa vifaa vya upasuaji na vingine vinavyoendana na hivyo. Ahsante.