Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mungu kwa kunipa uzima siku ya leo ili niweze kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na changamoto; kumekuwa na changamoto kubwa sana katika sekta ya afya katika Mkoa wangu wa Ruvuma. Elimu ya uzazi wa mpango bado inahitaji kufikishwa vijijini, vituo vya afya vingi havina maji, vituo vya afya havina magari ya wagonjwa jambo ambalo limekuwa likisababisha vifo vingi vya akina mama na watoto. Wahudumu katika vituo vya afya, manesi na madaktari ni tatizo kubwa.

Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wazazi kushirikiana na watu ambao wanawapa mimba wanafunzi kuwaficha wahalifu ambao wamewapa mimba watoto ambao ni wanafunzi. Je, Serikali imeshachukua hatua gani kwa wazazi ambao wanajihusisha na tabia hiyo ya kumdidimiza ntoto wa kike? Je, ni madume wangapi ambao wamefungwa kwa kosa la kumpa mimba mwanafunzi?

Mheshimiwa Naibu Spika, taa za kufanyia operation nazo ni shida, mashine za oxygen hakuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mbinga Mji kuna changamoto ya upungufu wa wodi za wagonjwa hususani wodi za akina mama (wodi ya wazazi),tunaomba Wizara itusaidie kuongeza wodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto nyingine ni kuhusu mikopo ya akina mama. Wanawake wamekuwa na hitaji kubwa la mikopo lakini hawapati ipasavyo, ipo mikopo inayotolewa na Halmashauri mbalimbali, lakini bado haitoshi. Je, Wizara ina mpango gani wa kuwawezesha wanawake?

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na vitendo vya kikatili ambavyo wamefanyiwa wanawake na watoto, hivi karibuni kuna mtoto ambaye anatembezwa kwenye mtandao ambaye ameshuhudia baba yake akiwachinja wadogo zake mapacha wawili. Napenda kujua kama Wizara inajua jambo hili na kama inajua imechukua hatua gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Wilaya ya Tunduru ina tatizo la kitanda cha upasuaji. Tunaomba Wizara ichukue hatua za haraka ili kuokoa maisha ya wananchi wa Wilaya ya Tunduru.