Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naunga mkono hoja, naomba nitoe mchango wangu kwa kuanza na suala la ukosefu wa gari la wagonjwa. Katika Halmashauri yangu ina vituo vya afya vya Serikali ambavyo ni Mtowisa, Laela, Miwepa, Mpui na Msanda Muungano. Vituo hivi havina gari la wagonjwa isipokuwa ni juzi tu Serikali ilitupatia gari la wagonjwa aina ya P-Suzuki gari ambalo kulingana na mazingira ya jimbo langu tuliamua kulipeleka Kituo cha Afya Laela. Hivyo tunaomba kwa kuanzia tena tupatiwe gari la Kituo cha Afya Milepa kituo ambacho kina msongamano wa wagonjwa na kina hudumia kata saba na kiko katika mazingira magumu kimiundombinu. Pili, ikiwezekana na Kituo cha Afya Mpui nacho kipatiwe gari la wagonjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu upanuzi wa vituo vya afya, tunashukuru Serikali kutupatia shiligi milioni 400 kwa ajili ya upanuzi wa kituo na kazi inaendelea vizuri, tatizo litakalobaki katika kituo cha afya hicho cha Milepa ni gari la wagonjwa. Tunaomba kutokana na jiografia ilivyo katika jimbo langu, naomba sana tupatiwe fedha kwa ajili ya upanuzi wa kituo cha afya Mpui.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu upungufu wa watumishi wa Wizara ya Afya katika Halmashauri yangu yapata asilimia 67 kwa maana ya waganga, wahudumu, wauguzi, manesi na kadhalika. Tunaomba Serikali ipeleke watumishi wa kutosha. Kwa upande wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, tunashukuru sana Serikali kututengea shilingi bilioni
1.5 kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Wilaya katika Wilaya ya Sumbawanga ambapo Halmashauri tayari ilishahamasisha wananchi kupitia Mkuu wa Wilaya Dkt. Haule akilishirikiana na viongozi wengine Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Madiwani. Hadi sasa tumeshafyatua tofali 400,000; pia kutenga eneo hekari 30, tunasubiri fedha zije tuanze kazi ya ujenzi, tunashukuru sana na naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika jimbo langu tunavyo vituo vya afya vinavyoendelea kujengwa kwa kushirikiana na wananchi kwa nguvu kazi na michango mbalimbali. Tunaomba Serikali itupatie fedha za kumaliza ujenzi wa vituo hivyo ambavyo ni Muze, Ilemba, Kaoze,Kipeta na Kalambanzite.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama sera ya Chama cha Mapinduzi inavyoelekeza kuwa na ujenzi wa zahanati kila kijiji wananchi waliitikia wito huo kwa dhati na kuanza kazi hiyo. Tunazo zahanati yapata nane ambazo zimefikia katika hatua ya mwishoni ili ziweze kusajiliwa na kuanza kutoa huduma, na ni kutokana na nguvu za wananchi, michango na kushirikiana na Mbunge wao kupitia Mfuko wa Jimbo ambazo ni zahanati ya Maleza, Mpona, Ilanga, Mumba, Jangwani, Kizumbi, Kazi na Mtapenda. Tunaomba Serikali kuunga mkono kwa kutoa fedha ili kumalizia zahanati hizo haraka ili ziweze kutoa huduma haraka kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na kutowakatisha wananchi hao tamaa. Zipo pia zahanati za wananchi ambazo ni kama zifuatavyo; Ngingo, Kawila, Ilambo, Ndelema, Mshani, Sikaungu. Zipo pia zahanati ambazo zilisha anza kutoa huduma, tunaomba Serikali itoe fedha za kuboresha kwa kumalizia majengi zahanati hizo ni Kisa, Msia, Sakalilo, Kisa, Lyapona, Ilembo, Kinambo.