Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa maoni yangu juu ya hoja ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna upungufu mkubwa wa wataalam wa sekta ya afya karibu zahanati, vituo vya afya na hata hospitali za mjini na vijijini. Hili jambo ni kubwa naomba Serikali ilifanyie kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mahusiano makubwa ya TAMISEMI na Wizara ya Afya hivyo ni maoni yangu kuwa kuwe na chombo cha pamoja kushughulikia allocation ya watumishi wa afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna shida ya wazee kupata matibabu kwa kutumia bima au utambulisho kwa wazee.

Hili jambo naomba lifanyiwe kazi ili wazee wasipate shida pindi wanapougua.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna shida kubwa ya gari la wagonjwa katika hospitali, vituo vya afya Ilala na hasa Jimbo la Ukonga. Naomba nipate gari la wagonjwa walau lihudumie Ukonga tu ili kuwa na uharaka wa usafiri pindi tupatapo wagonjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.