Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Jambo la kwanza nitumie fursa hii kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nzega kuishukuru Serikali kwa dhati kabisa kwa support ambayo imetupa katika improvement ya Kituo cha Afya cha Zogolo, lakini vilevile mpango uliopo kwa ajili ya vituo vya afya vya Mbogwe na Migua. Pia nimshukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, na nikushukuru kwa dhati kabisa Mheshimiwa Ummy kwa kazi kubwa unayoifanya kuhakikisha kwamba akina mama wanajifungua wakiwa salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nilitaka nishauri mambo mawili madogo. Improvement tunayoifanya katika referral hospital, kwa mfano kama Muhimbili Serikali imafanya kazi kubwa sana ya ku-improve hospitali yetu ya Muhimbili na dhamira ya Wizara kuhakikisha kwamba akina mama wanajifungua salama nilitaka niiombe Serikali Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Afya na Wizara ya Mzee Mkuchika kutumia takwimu za TASAF, zile kaya maskini, ili tuweze ku- establish akina mama wanaotoka katika kaya maskini kabisa kuona au kuja na mpango wa namna gani wanaweza kupata zile delivery kits ili wasiweze kukumbana na lile zoezi la kuwa wanalipa shilingi 20,000 ama kwenda kununua kwa sababu kuna kaya ambazo ni maskini na kwa takwimu zetu kuna asilimia kama 28 mpaka 30 ya Watanzania ambao wako katika umasikini wa hali ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ambalo nilitaka niiombe Wizara, MSD tunatenga fedha za dawa nyingi lakini bado kuna tatizo la out of stock. Nikitolea mfano katika Wiaya ya Nzega na Mheshimiwa Waziri wewe mwenyewe uliliona katika ziara yako hivi juzi tulivyokwenda wote, mtu ana
bima, anafika katika dirisha anakosa dawa, ina-discourage watu kujiunga katika National Health Insurance. Mfano, jambo la pili ambalo ni la kusikitisha, tunaamini MSD wako katika mfumo ambao unawafanya waombaji wa dawa kuweza kupata feedback haraka ya kujua kwamba dawa hakuna lakini kupata ile barua ya kuwaruhusu kwamba we are out of stock, hatuna dawa kwenda kununua dawa katika vendors ambao mmewaruhusu inachukua ages.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi leo hapa mkononi nina barua iliyoandikwa na Daktari wa Hospitali ya Wilaya Nzega tarehe 27 Februari, aliomba idadi ya dawa tofauti 100. Kati ya hizo 100 akakosa 48, ile barua ya kumruhusu ili aende kwa vendors ili aweze kwenda kununua hizo dawa 48 tofauti mpaka leo hawajapata. Matokeo yake inaonekana kwamba fedha tunazotenga, wananchi wanaokwenda kupata dawa katika viuto vyetu vya afya ama hospitali zetu wanakuwa hawapati dawa kwa sababu ya inefficiency ya taasisi zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi nilitaka niiombe Serikali, tunatenga fedha kama Bunge na zile dawa muhimu ukiangalia bajeti ya mwaka jn ni almost asilimia 100 hazina wametoa fedha zake lakini zile dawa kuzipata kwa wakati katika vituo vya afya ni changamoto. Mimi niwa- challenge Serikali, tafuteni solution ya MSD na delivery system katika vituo vyetu vya afya kuhakikisha kwamba kinachoombwa kinapatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi teknolojia imekua mtua anaweza akaomba kutokea ofisini kwake akajua stock iliyopo na ambayo haipo, system ikamruhusu kwenda kuomba katika vendors waliopo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, otherwise mimi nitumie nafasi hii kuwashukuru sana na naunga mkono hoja, ahsante sana.