Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi na mimi siku ya leo niweze kutoa mchango wangu kwenye Wizara hii ya Afya na ninaomba nianze tu na suala zima la upungufu wa wahudumu wa Wizara ya Afya na naomba nilisemee kwa Mkoa wa Dodoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Dodoma ni Mkoa ambao umekwenda sasa kupata ongezeko kubwa sana la wageni kutoka nje na tuna Hospitali ya Rufaa kwa maana ya Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, lakini pia tuna Hospitali ya Benjamin na hospitali zingine za taasisi, lakini kumekuwa na changamoto kubwa sana ya foleni ama msongamano kwenye hospitali hizi. Nilikuwa nataka Mheshimiwa Waziri ukija naomba utuambie wananchi wa Dodoma msongamano huu, mkakati wako ni nini wa kuepusha msongamano kwani watumishi kwa maana wageni wengi ambao wameingia ni watumishi wa Serikali na mara nyingi wanatumia kupata appointment na madaktari wanapofika pale hospitalini hawapangi foleni. Wenyeji wa Mkoa wa Dodoma wanapanga foleni Mheshimiwa Waziri mpaka siku tatu mtu hawezi kumuona daktari, kwa hiyo naomba Mheshimiwa Waziri utakapokuja uweze kuniambia suala hilo linatatuliwaje kwa udharura wa ongezeko la watu katika Mkoa wetu wa Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba kusemea suala zima ni sera ya Serikali kwamba kila mkoa unatakiwa kuwa na Hospitali ya Mkoa, Wilaya kuwa na Hospitali ya Wilaya, lakini pili kata kuwa na vituo vya afya na vijiji kuwa na zahanati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wengi wamekuwa wakisimama hapa wanalalamikia suala zima la hospitali za Wilaya na vituo vya afya. Mkoa wangu wa Dodoma una Wilaya saba, Wilaya tatu hatuna hospitali. Tumekuwa tukiomba fedha mara kadha wa kadha na fedha hizo hazitoki. Sasa Mheshimiwa Waziri suala la ongezeko la watu hapa Mkoa wa Dodoma linakwenda pia kuleta changamoto kubwa kwa sababu wananchi wa Wilaya za pembezoni zote wanapokosa huduma huko kwenye Wilaya zao wanakuja hapa Makao Makuu kwa maana ya Hospitali ya Mkoa wa Dodoma. Sasa leo Wilaya hizi hazina hospitali za Wilaya, lakini bado kuna msongamano mkubwa, naomba utuambie Mheshimiwa Waziri hizi Wilaya tatu nini hatma yake kwenye bajeti hii ya fedha ya mwaka huu 2018/2019. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Chemba ina kata 26. Kati ya kata 26 ni kata nne tu ndiyo ina vituo vya afya, lakini tuna kituo cha afya Kituo cha Hamai, kituo hiki nilikisemea Bunge lililopita ama kikao cha bajeti kilichopita. Hiki ndiyo kituo kinachotumika kama Hospitali ya Wilaya ya Chemba, lakini cha kustaajabisha na cha kusikitisha kituo hiki kina watumishi 16, kituo hiki hakina maji, kituo hiki hakina x-ray machine, kituo hiki hakina gari la wagonjwa. Kituo hiki acha tu kwamba kinahudumia kama kinakuwa kina-take charge ile ya wagonjwa wa Wilaya ya Chemba, lakini pia kinahudumia Wilaya ya Kiteto, kinahudumia Wilaya ya Chamwino, kinahudumia Wilaya ya Kondoa. Hivi vitu hebu tunaombeni muwe mnatuona na watu wengine huku, msiwe mnagawana gawana tu hizi fedha halafu watu wengine mnatusahau. Mngeacha hata kutujengea ule uwanja wa Chato kwa shilingi bilioni 42 mkatuletea hizi fedha zingeweza kutusaidia kujenga hizi hospitali zetu za Wilaya ikaweza kusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hii shilingi trilioni 1.5 ambayo inapigwa pigwa chenga na Serikali mimi naamini ipo mahali, mlikuwa mnatikisa kiberiti, sasa tunaomba muitoe hadharini ije iende ikatekeleze shughuli za maendeleo kwa kutoa huduma ya afya, kwani tunaamini Mama Salma amesema kwamba bila afya hakuna uchumi. Mnatangaza Serikali ya viwanda, Serikali ya viwanda Watanzania wagonjwa hawana dawa, hakuna wahudumu, Tanzania ya viwanda iko wapi?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ninaomba sana kwa jinsi mnavyojinasibu Serikali sikivu tunaomba usikivu huo uende kwenye shilingi trilioni 1.5 ikatuletee madawa na kulipa mishahara ya watumishi katika Taifa letu ili Watanzania waweze kwenda kuendelea.