Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuweza kunipatia nafasi nami kuchangia Wizara hii muhimu kabisa, na mimi niseme niweze kusikika na Mheshimiwa Waziri aweze kuona namna ya kusaidia mambo mengine.

Kwanza kabisa, nampongeza Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayofanya katika sekta mbalimbali ikiwemo Sekta ya Afya kwa sababu pamoja na kwamba tunapitisha, bajeti lakini Serikali ndiyo inatoa pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, naipongeza Wizara, Waziri, Naibu na Watendaji wake Wakuu. Ile sera ya kuboresha vituo vya afya; Kituo cha Kinyambuli tulipata shilingi milioni 400 na kinaendelea vizuri kabisa. Pia tangu niingie Bungeni nimekuwa nikijadili sana suala la Wilaya mpya kutokuwa na Hospitali za Wilaya. Kwa hiyo, nashukuru sana tumeweza kupata shilingi bilioni 1.5 mwaka huu na tunaenda kujenga Hospitali ya Wilaya. Huo ni ukombozi mkubwa sana kwa wana Mkalama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaendelea, yako mambo ambayo pia ni muhimu ukisimama uweze kusema. Kama liko jambo lina trend kwenye mtandao halafu unakaa kimya na unaona linaharibu sura ya Serikali, hatuwezi kukaa kimya.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana tunaona kwamba hapa na pale watu wanajaribu kutoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo. Sisi sote kama Waheshimiwa Wabunge tunajua kwamba Ripoti ya CAG inapotolewa, hizi oversight committees pia kama PAC, LAAC na PIC tutakaa na tutaleta ripoti Bungeni na ripoti hiyo itajadiliwa. Kwa hiyo, ni vyema watu wakatambua hilo. Huwezi ukamnyooshea mtu kidole au unamtukana halafu akawa amekaa kimya. Kwa hiyo, Kauli ya Serikali imekuja muda muafaka kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakupongeza, kama watu wameona kwamba ulivyopunguza muda wa maswali halafu karuhusu Kauli ya Waziri ili wananchi waone, kama wao wameenda kwenye mitandao, sasa umefanya kitu gani cha ajabu? Hilo ni jambo la lazima. Unajua watu wanasema mkuki kwa nguruwe...Sasa jambo hilo ni muhimu na uendelee kufanya hivyo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiendelea na uchangiaji katika hoja ya Wizara, Mheshimiwa Waziri lipo suala la Hospitali ya Kansa ya Ocean Road. Hospitali hiyo ni muhimu sana na wananchi wetu wanapata huduma muhimu.

T A A R I F A . . .

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, hata hivyo, taarifa hiyo siipokei kwa sababu wao wanapenda kusema halafu sisi tusiseme. Sasa tutasema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Ocean Road inatoa huduma, nzuri lakini wananchi wetu wanapata shida sana. Mheshimiwa Waziri umekiri kwenye ripoti yako kwamba waiting time ni wiki sita watu kupata huduma pale, mnataka m-reduce mpaka wiki mbili. Sasa kuna mitigation gani inafanyika hapo ndani ya wiki sita na watu wanapoteza maisha? Mheshimiwa Waziri unajua kabisa nimeshapoteza wananchi wangu wa Mkalama kwa kusubiri huduma hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni suala la dawa. Mheshimiwa Waziri umezungumza suala la duka la dawa kuwa na dawa toshelevu. Tunaomba jambo hilo liwekewe mkakati, bajeti iwekwe ya kutosha kwa sababu yako maduka nje ya Muhimbili ambayo yanauza hizo dawa kwa bei ghali na wananchi hawawezi kumudu gharama hizo. Sasa jambo hilo linachafua taswira ya Ocean Road na inaonekana kama ni jambo la makusudi na kwa bahati mbaya daktari hawezi kusubiri mgonjwa afe anamwambia nenda mahali fulani utapata dawa. Picha wanayopata wananchi ni kwamba hayo maduka ni ya madaktari husika. Kwa hiyo, tunawapaka matope madaktari wetu na jibu sahihi ni hospitali yetu kuwa na dawa za kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri natambua kabisa kwamba TAMISEMI wanaweza kutupatia gari na labda Halmashauri inaweza kununua. Nimekuwa nikizungumza sana suala la ambulance.

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi juzi tu ametokea Diwani wangu mmoja amepata stroke, amecheleweshwa hospitali kwenda Singida kwa sababu hakuna usafiri, na mimi ni Mbunge. Sasa tunaomba jambo hilo kwa vyanzo vyovyote vile tuweze kupata gari la wagonjwa. Mkalama hatuna gari la waonjwa. Lile ambalo lilijibiwa na TAMISEMI ni gari lililochoka, Wilaya ilivyogawiwa tulipewa, linatugharimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuokoe maisha ya wananchi. Tunaomba tufikiriwe kwa jambo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala zima la hoja za watumishi wa afya…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji