Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami nichangie kidogo kwenye Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nataka niseme kwamba, bajeti ya dawa kwenye Wizara hii imechukua sehemu kubwa ya bajeti nzima. Kwa hiyo inaonesha kabisa kwamba kwa kuchukua bajeti hii kubwa ya dawa, kwamba Serikali hii imejipanga kutibu zaidi watu kuliko kuwapa kinga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niongelee kidogo kuhusiana na Mkoa wangu wa Katavi. Mkoa wa Katavi sasa hivi sisi ni vinara kwa watoto wadogo wa kike wanapata mimba za utotoni kwa zaidi ya asilimia 36.8. Kwa hiyo ningeomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha atueleze kwamba, kama Wizara na Serikali kwa ujumla wana mkakati gani wa kuhakikisha hawa vijana au watoto wadogo wa kike wanapata elimu ya uzazi wa mpango, ili tupunguze hili janga katika Mkoa wetu wa Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu tu, watoto wa kike wsichana 624 ambao wako chini ya umri wa miaka 18 kwa mwaka wanajifungua katika hospitali zile zile zilizopo katika Mkoa wetu wa Katavi, hatuna hospitali ya mkoa, tuna hospitali ya wilaya na hizi zahanati ndogo ndogo. Hata hivyo pia zahanati hizi pamoja na hospitali ya wilaya zimekuwa zikibeba mzigo mkubwa. Upungufu wa watumishi unasababisha watumishi hawa kufanya kazi wana-over late, wanafanya kazi na malipo yao pia, bado wanawacheleweshea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Waziri kwa kuangalia uzito wa jambo hili, mimba za watoto katika Mkoa wetu wa Katavi limekuwa ni tatizo kubwa na watumishi pamoja na Madaktari, Wauguzi, pamoja na Manesi wanafanya kazi kubwa sana. Hakuna wodi za kutosha; akinamama wanalala wawili wawili kwenye vitanda. Kwa kupitia hii Serikali ya viwanda sasa wajipange na si kupeleka tu pesa kwenye mambo yasiyo na msingi, waangalie vipaumbele vya Watanzania kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ujenzi wa hospitali ya mkoa. Kama nilivyosema na nimekuwa nikiongelea sana jambo hili. Pesa ilitengwa zaidi ya bilioni moja, lakini mpaka sasa hivi haieleweki zile pesa ziko wapi. Kwa hiyo, tunaomba kupitia Wizara jambo hili hebu likae wazi, pesa hizi zirudishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkurugenzi huyu, Mchina aliyehusika kupiga hizi pesa pamoja na Baraza la Madiwani lililopita waeleze pesa hizi ziko wapi, kwa sababu wanawapa mzigo watu wa Mkoa wa Katavi wanasafiri kutoka Mpanda kwenda Mbeya kufuata huduma kwenye hospitali za rufaa. Kwa hiyo, watu hawa wasiendelee kuwapa matatizo watu wa Mkoa wa Katavi, watu wanatumia gharama kubwa, wanasafiri siku nyingi kufuata huduma za rufaa katika Mkoa wa Mbeya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nijue tu Serikali wamejipangaje, kwa sababu takwimu zinaonesha kwamba afya ya akili kupitia Hospitali yetu ya Milembe, wagonjwa wanaongezeka kwenye hospitali hiyo. Sasa kama Serikali wamefanya utafiti gani kuona kwamba kwa nini Watanzania wengi kupitia haya magonjwa ya akili wanaongezeka katika Hospitali ya Milembe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Tanzania pia, ni nchi ya tatu ambayo inaongoza kwa udumavu na ni nchi ya 10 inayoongoza kwa udumavu uliokithiri. Sasa ningeomba tu, kwamba kwa takwimu hizi tukielekea kwenye Serikali ya viwanda na tunategemea kwamba hawa ni watoto, maana yake watakwenda shuleni tunakwenda kuzalisha watoto ambao watakuwa na utapiamlo, watoto ambao watakuwa na udumavu wa akili, hawatapata elimu ya kutosha. Sasa hiyo Serikali ya Viwanda bila kuwekeza kwenye elimu kupitia hawa watoto kupata lishe bora tunakwenda kutengeneza Taifa la namna gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakiniā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)