Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana nimepata nafasi hii, Mungu akuweke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa sisi Wabunge sita tuliopata ajali Morogoro, lakini sote tuko salama na amani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nawashukuru watu wa Hospitali ya Morogoro, wananchi wake na madaktari wametuhudumia mara moja. Vilevile nawashukuru Hospitali ya Muhimbili na hospitali tuliyohamishiwa MOI Hospital.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nawashukuru watu wa NHIF (watu wa Bima ya Afya), wameleta ndege mbili, ambulance nne, tumepata nafasi nzuri ya kupelekwa hospitali na tumepata huduma nzuri. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu na tunamshukuru Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tunamshukuru Waziri wetu, Mheshimiwa Ummy, pamoja na Naibu wake, wamekuja hospitali kutuona, ametupa pole.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru Waheshimiwa Wabunge wote wa Bunge letu hili, nawashukuru pamoja na watu wangu wa Jimbo, wamekuja kuniona katika hospitali. Kwa hiyo, nasema kwa wote, ahsante sana.