Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mungano na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Jamal Kassim Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mungano na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kunipa nafasi, acha nijielekeze moja kwa moja kwenye kuchangia hotuba na mimi nitajiekeza kwenye suala la mikopo ya nje. Suala la mikopo ya nje linasimamiwa na Serikali ya Muungano, ni suala la Muungano. Kumekuwa na ucheleweshaji wa muda mrefu sana kupatia approval miradi ya kimkakati ambayo inafanyika kupitia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe ni shahidi, jengo la Terminal II katika Uwanja wa Amani Abeid Karume International Aiport limesimama toka mwaka 2014. SMZ imeomba extension ya mkopo kwa ajili ya kukamilisha mradi ule lakini mpaka leo hii bado. Sote tunajua uchumi wa Zanzibar unategemea utalii na bila kuwa na airport kubwa yenye uwezo hatuwezi kufikia lengo lile ambalo tumejiwekea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchumi wa Zanzibar kwa takribani 40% unachangiwa na sekta ya utalii. Matarajio ya Zanzibar ni kupokea mwakani wageni wapatao 500,000. Kwa infrastructure iliyokuwepo pale haitoshi. Tunaomba kabisa suala la approval ya mikopo hii lifanywe kwa wakati na kwa haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini siyo hivyo tu, tuna mradi mwingine wa Bandari ya Mpigaduri. Kwenye Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015 tumeahidi katika kipindi cha miaka mitano hii tutajenga Bandari ya Mpigaduri kwa ajili ya mizigo, lakini mpaka leo bado approval za mikopo hii haijatoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu miradi hii mikubwa miwili ni toshelezi kabisa kwa kusaidia uchumi wa Zanzibar. Kukamilika kwa miradi hii kutaufanya uchumi wa Zanzibar kuimarika, lakini si kuimarika kwa uchumi wa Zanzibar tu, pia kuimarika kwa uchumi wa Tanzania kwa ujumla wake. Uchumi wa pande zote hizi zina-compliment each other, tunajua mizigo itakayoshushwa Bandari ya Mpigaduri mingine itaenda Rwanda, Burundi, Zaire, Congo lakini itaenda kupitia wapi, itapitia Bandari ya Dar es Salaam. Kwa hiyo, niombe sana Mheshimiwa Waziri aje atuelezee nini hasa tatizo katika approval ya mikopo hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini eneo lingine ni suala la biashara ya pamoja. Mimi naamini kabisa moja ya sababu kubwa na faida za Muungano wetu ni fursa za biashara kwa upande wa Zanzibar kuja Bara na upande wa Bara kwenda Zanzibar. Ukifanya trade analysis, hizi changamoto za leo miaka ya 1990 hazikuwepo. Ukichukua analysis za miaka ya 1990 Zanzibar ilikuwa inauza zaidi Bara kuliko Bara inavyouza Zanzibar. Nimeona jitihada ambazo Waziri anasema kuna ZBS na ZFDA, lakini kwa nini haya mambo yako upande mmoja tu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitu vikija Bara ndiyo kunakuwa kuna TBS na TFDA lakini vitu vya Bara vinakuja Zanzibar bila ya haya matatizo. Hizi changamoto zimechukua muda mrefu kutatuliwa. Kwa hiyo, mimi pia nimuombe Mheshimiwa Waziri, hili suala alitizame kwa upana na uzito wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuzungumza ni suala la kodi ya foroddha. Kodi ya Forodha iko kwa mujibu wa utaratibu. Leo hii ukienda kukaa Bandari ya Dar es Salaam pale, watu wanaotoka Zanzibar, mtu akinunua kitu chake kidogo tu akifika pale anatozwa kodi. Unajiuliza hizi base za kodi wanazotozwa ni zipi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mfano hai, juzi kuna mwananchi wa Jimboni kwangu amesafiri na cherehani moja tu, amefika Bandari ya Dar es Salaam ametakiwa alipe shilingi 100,000. Cherehani ya shilingi 200,000 Dar es Salaam, alivyofika bandarini ametozwa shilingi 100,000. Kwa hiyo, haya tunayoyazungumza ni muhimu sana yatizamwe na haya mazungumzo yanazungumzwa nenda, rudiā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)