Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naushukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza ndugu yangu Mheshimiwa Jafo na Naibu Mawaziri wote wawili wa Wizara hii kwa kazi kubwa wanazofanya na kujituma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilitaka nianze kwa jambo moja; jamii yoyote inayohitaji maendeleo msingi mkubwa wa maendeleo ni haki na viongozi kujua kwamba wana wajibu wa kulinda uhai na mali za kila raia. Nasema hivi kwa sababu kumekuwa na hii culture ya impunity na matukio madogo madogo yanayoendelea, na mimi kwa mtazamo wangu naamini kwamba it is a high time Serikali ikaja hadharani na kuteka bold decision juu ya haya mambo ambayo yamekuwa yakiendelea katika jamii yetu; kwa sababu yanaharibu taswira na heshima na jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka niongee kuhusu TAMISEMI. Ukitazama taarifa ya Waziri only 40 percent maximum of 50 percent ya Development Budget ndiyo imekwenda kwenye Halmashauri zetu. Hata hivyo katika Halmashauri zetu mapato yetu ya ndani yanaathirika sana pale ambapo Central Government inashindwa kushusha fedha kwa wakati katika Halmashauri, na kule ndiko ambako kuna burden kubwa iliyopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kisera tumeamua kuwa na D by D, naomba nitumie takwimu hizi kuwaonesha Waheshimiwa Wabunge. Katika sekta ya elimu ukichukua ratio ya pato letu la taifa vis-a-vis kile ambacho tuna-allocate katika sekta; kati ya mwaka 2006 mpaka 2007/2008 ratio ilikuwa ni asilimia 20 ya pato letu la ndani ndiyo ilikuwa allocated kwenye sekta ya elimu. 2009 na 2010 ikawa asilimia 18. Imeendelea kushuka, mwaka 2017/2018 tumetenga only 15 percent ya pato letu la ndani kupeleka kwenye sekta ya elimu, sasa nini implication yake?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitazama matokeo ya kidato cha nne asilimia 60 ya wanafunzi wanaomaliza mtihani wa kidato cha nne wanafeli; na ni kwa nini? Kwa sababu kwa takwimu, na hizi ni takwimu za BEST, satisfaction ya walimu, job satisfaction only 30 percent ya walimu walioko katika shule zetu za msingi na sekondari ndio wako satisfied na kazi wanayoifanya, maana yeke tunaandaa janga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini fedha za elimu tunazozipeleka TAMISEMI, asilimia 96 ya fedha hizi zinatumika kwenye administrative only, haziendi kwenye development ya education, kwa maana ya kujenga infrastructure na kuangalia stahiki za watoa elimu, hili ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna umuhimu mkubwa sana Serikalini wa kufanya replanning, nini focus yetu? Tunataka kujenga uchumi wa viwanda. Ili tujenge uchumi wa viwanda ni mambo mawili tu, moja ni uwepo wa rasilimali kwa maana ya raw material, lakini uwepo wa rasilimali watu. Kama elimu yetu matokeo yake ni haya ni matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwape mfano wa TARURA; mwaka jana tumetenga shilingi bilioni 246, mwaka huu tunatenga shilingi bilioni 272. Ukitazama mipango yetu ya maendeleo ni urban centric, yote inatazama Dar es Salaam, Mbeya, fedha zinaenda Jiji la Mwanza na vitu vya namna hiyo, lakini kule ambako kuna wazalishaji wa rasilimali, kwa maana ya wakulima, barabara zao tumeziweka chini ya TARURA, hatuzipi fedha ama tunachoki-allocate ni kidogo, tuna matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kuhusu suala la TARURA; Waheshimiwa Wabunge wamesema tuangalie hela ya mafuta 30 percent kwa ratio ya 70 percent, ninaomba Wizara ya Fedha angalieni kutumia chanzo cha Gaming Board, chanzo hiki kiwe dedicated kisheria, kiende moja kwa moja kuongeza Mfuko wa TARURA. Pamoja na ratio mnayoitumia sasa hivi tumieni Gaming Board kuna fedha, watu wana-bet. Tumeamua kuruhusu watu wacheze kamari, basi tumle huyu nguruwe vizuri aliyenenepa ili matokeo ya kule yaje basi kwenye barabara, hili ni eneo lingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 52 anasema; ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi Tanzania unategemea kwa kiasi kikubwa sekta ya kilimo. Sekta hii ni mhimili wa uchumi wa viwanda na kuchangia kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati. Ili tuweze kufikia lengo hili ni lazima tuwekeze kwenye sekta ya kilimo, tutoe fedha za pembejeo, tujenge barabara za kutoa mazao kwa wakulima vijijini kuleta kwenye barabara kubwa zilizojengwa na TANROADS, bila kufanya hivi hatuwezi kutatua hili tatizo la kuondoa umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niiombe Serikali. Leo kule kwenye Halmashauri, na mimi nasema hii kwa nia njema, kule kwenye Halmashauri Serikali kwa maana ya Rais amekuja na vision kubwa kupambana na rushwa, kujenga miundombinu, kuhakikisha kwamba wananchi masikini wanapata haki, lakini ukitazama kinachoendelea katika Halmashauri zetu, ni kero kubwa kwa wafanyabiashara wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mkulima kabeba mpunga wake kutoka Katavi kwenye gari la tani 10 kaamua kufunga yale magunia kilo mia-mia badala ya kilo 90, lakini uzito ni tani 10, akifika njiani anapigwa faini. Msafirishaji wa ng’ombe kutoka Nzega kuleta Dar es Salaam, amekatiwa ushuru, ana leseni, ana kila kitu, akifika njiani kasimamishwa kapigwa fine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaongoza Halmashauri na nchi kwa faini, hatuwezi kuwasaidia hawa watu maskini. Ningemuomba Mheshimiwa Waziri Jafo wakati anakuja kufanya winding up hapa atuambie definition, kuna mgogoro mkubwa unaendelea kwenye Local Government. Tulipitisha hapa Waziri wa Fedha alileta Mabadiliko ya Sheria ya Fedha mwaka jana, wenye hoteli ambao wanalipa VAT je, wanatakiwa walipe service levy? Je, wanatakiwa walipe hotel levy?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu sasa hivi kinachoendelea analipa VAT, anapelekewa service levy anapelekewa hotel levy, asipolipa anafungiwa. This is a very bad thing, na mimi nataka niseme Waheshimiwa Wabunge wa chama change, kwamba tunaweza tukajenga standard gauge, tunaweza tukanunua ndege, tunaweza tukajenga barabara, kama kero zinazohusu maisha ya watu ya kila siku hatutakuwa wakali kuitaka Serikali ichukue hatua mapema, sisi ndio tutakaoenda kunyooshewa vidole. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kule kwenye Halmashauri kila mtu ni mbabe. Mtu ana kabisahara ka-shilingi 500,000 anapigwa fine ya shilingi 2,000,000, It is very unfair. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo ambalo nakuomba kabisa ndugu yangu Mheshimiwa Waziri Jafo toka strong statement. Hii tabia ya Wakurugenzi wetu kwenda kufungia watu makufuli, kwenda na polisi kuburuza, unaletewa sasa hivi demand note, in a next one hour umepigiwa kufuli. Demand note inasema nini, hujalipa service levy… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante.