Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia suala la maji lililopo katika Jimbo langu. Katika Kata ya Kanyangereko, Vijiji vya Butahyaibega, Bulinda wakati wa kiangazi wanapata shida sana mito inakauka. Hivyo akinamama wanapata shida sana na kauli ya Serikali ni kumtua mama ndoo kichwani. Sambamba na Kata ya Bujugo, Rubafu na Maruku, shida ni hiyohiyo ya maji safi na salama. Naomba suala hili la maji litafutiwe ufumbuzi maana ni kila mwaka shida hii inajitokeza, sijui Serikali itawasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu Wizara ya Mifugo na Uvuvi; je, ni lini Serikali itawapiga marufuku wafugaji kulisha mifugo yao barabarani kwa sababu inaweza kusababisha ajali kwa madereva na sehemu zingine imekwisha tokea. Hivyo, naomba lishughulikiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kuuliza, je, ni lini Serikali itakarabati barabara zilizo chini ya kiwango.