Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa miradi ya maendeleo hususan miradi ya ujenzi. Nashauri:-

(i) Kandarasi zitolewe kwa ushindani lakini kwa kuzingatia fursa maalum kwa makampuni ya wazalendo na wataalam wazalendo – Wakandarasi, Wahandisi Washauri, Wabunifu na Wakadiriaji Wajenzi na kadhalika. Hii itaboresha zaidi.

(ii) Kujenga uwezo wa ndani ya nchi kwa ajili ya matengenezo (maintanance) ya miradi hiyo na miradi mipya.

(iii) Kuiwezesha sekta kuchangia zaidi uchumi wa nchi na kadhalika.

(iv) Miradi mikubwa yote itumike kama madarasa (vituo vya mafunzo) kwa vitendo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu , vyuo vya kati lakini pia kwa wahitimu wa shahada na stashahada kupitia bodi ili kuhamishia ujuzi na utaalam kwa vitendo nchini. Mifano, bomba la mafuta - Hoima, Stiegler’s Gorge - umeme, madaraja makubwa, viwanja vya ndege vikubwa, reli – Standard Gauge(SGR), majengo makubwa na yenye mahitaji mahsusi na kadhalika.