Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na hotuba ya Waziri Mkuu inayohusiana na mapitio na mwelekeo wa kazi za Serikali na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha za Ofisi yake na ya Bunge kwa mwaka 2018/2019, naomba nichangie kwenye huduma za jamii kipengele cha elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba ya Waziri Mkuu imeonesha kuna mafanikio makubwa ya mpango wa utoaji elimu ya awali na msingi bila malipo. Katika maelezo yake imeonesha Serikali imekuwa inapeleka fedha zote za ruzuku moja kwa moja katika shule zetu. Sisi wawakilishi wa wananchi katika maeneo yetu tunayotoka fedha hizo hazifiki kwa wakati na pia hazitoshelezi mahitaji ya shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mfano hai wa Jimbo la Manispaa ya Iringa, kuna baadhi ya shule ambazo ruzuku hii haitoshelezi mahitaji yao. Mfano wameshindwa kumlipa mlinzi wa Shule ya Msingi Azimio kwa muda wa mwaka mmoja na miezi mitatu, pia maji yamekatwa wanafunzi wa shule ya awali hawapati uji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika ongezeko la kuandikisha watoto shule za msingi naona imeshuka kutoka 2,120,667 mwaka 2017 hadi kufikia 2,078,379 mwaka 2018. Je, hili ni ongezeko?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri tusiweke siasa katika elimu kwa sababu elimu ni ufunguo wa maisha.