Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, napenda kuchangia kuhusu gratuity ya Waheshimiwa Wabunge. Kukata kodi gratuity ya Waheshimiwa Wabunge siyo sahihi kabisa kwa kuwa kwa sasa tunakatwa kodi kwenye mishahara yetu. Nashauri wakati wa Finance Bill ondoeni kodi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni lini agizo la Mheshimiwa Rais la kushusha riba katika taasisi za fedha litaanza ili wananchi wetu wakope na wakuze uchumi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, pitieni upya mgawo wa fedha za elimu bure kwani hazitoshelezi kuendeleza shule zetu