Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza sana juhudi za Serikali kwa kazi nzuri zinazofanyika kwa ajili ya manufaa ya wananchi. Naipongeza sana Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kazi nzuri hasa katika kuwezesha wananchi kuongeza kipato kwa kupitia mikopo kwa vijana na vikundi vya wanawake, SACCOS na VICOBA. Ushauri kwa Serikali, naomba Serikali kujenga Hostel kwa kila sekondari ili watoto wetu waweze kukaa shuleni na kuepukana na kupata mimba kwa watoto wa kike na kuongeza kiwango cha elimu kwa watoto wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, naishauri Serikali ipeleke umeme kila Shule ya Msingi na Sekondari, ijenge miundombinu ya shule kama vile ujenzi wa vyoo vya shule, nyumba za Walimu pamoja na kumalizia maboma ya madarasa ambayo wananchi wameshajenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kilimo, Serikali ipeleke mbolea na mbegu kwa wakati au kwa kufuata kalenda ya kilimo. Pia ilipe deni la Wakala ambao bado hajalipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile Serikali itatue tatizo la maji hasa vijijini na kuongeza Mfuko wa Maji ili bajeti ya Wizara ya Maji iwe inatosha. Pia kuanzisha Bodi ya Maji kila Wilaya; kuwe na chombo ambacho kitafuatilia utekelezaji wa miradi ambayo Serikali imeshapeleka fedha nyingi na miradi hiyo haijakamilika. Serikali imalizie maboma ya Vituo vya Afya na Zahanati ambazo bado hazijakwisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.