Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kazi na Ajira (Workers Welfare Viwanda vya Mafinga). Mafinga ina Viwanda vingi vya mazao ya misitu, lakini hali za wafanyakazi ni duni (welfare). Mbaya zaidi wafanyakazi wakipeleka malalamiko Ofisi ya Mkuu wa Wilaya taarifa
zinarudi kwa mwekezaji kumsemea mlalamikaji kuwa ni mtu mbaya, matokeo yake, mfanyakazi anatafutiwa visa anafukuzwa kazi na kwa lugha ya kejeli anaambiwa nenda popote. Naomba na kushauri, Mheshimiwa Waziri afanye ziara ya kushtukiza na akifika aongee na wafanyakazi, asiishie kupokea taarifa ya menejimenti au ya uongozi wa wilaya tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji wanapaswa kuwathamini wafanyakazi, OSHA wasiishie tu kuchukua tozo bali wafanye serious ukaguzi, mazingira ya kufanyia kazi ni mabaya, is completely against labour rights. Kwa mfano, kuna kazi ya kupanga magogo, wafanyakazi hawana gloves, hawana mabuti, wamevaa kandambili, hawana kofia, ni mazingira hatarishi. Hawana usafiri, mtu anatembea kilometa nne hadi tano kwenda kazini a total of eight to ten kilometers.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchumi wa viwanda uendane na hali bora za wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.