Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kwanza kumshuku Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo. Nilichangia kwa kuongea, naomba nichangie kwa maandishi kwa eneo ambalo sikumalizia na kuweka kwa muhtasari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashauri Waziri wa Fedha aweze kupatiwa fursa tena ya kutoa msamaha wa kodi katika eneo la miradi ya kitaifa na miradi mbalimbali ya jamii ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; marekebisho ya sheria yaje mapema Bungeni turekebishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nashauri Serikali iangalie namna bora ya kuweka vyanzo vya mapato vya uhakika katika Mfuko wa Mazingira. Si tozo mpya bali kutokana na ada, tozo, ushuru na leseni mbalimbali asilimia fulani ziende katika Mfumo wa Mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni suala la kuwa na vyanzo vya mapato kwa ajili ya Mfuko wa UKIMWI na watu wenye mahitaji maalum. Pia halmashauri zitoe mikopo kutokana na ile asilimia 10 ya vijana na wanawake kwa wenye mahitaji maalum na wenye Virusi Vya UKIMWI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Serikali iangalie ushauri wa kuongeza Sh.50/= kwa kila lita ya mafuta ili iwe Sh.100/= kwa kila lita ya mafuta. Pia kuondoa kodi kwenye mitambo ya kuchimba maji, pampu za maji zenye mita na pampu za maji za sola. Hii itafanya gharama za vifaa hivyo na huduma ya uchimbaji kupungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Sheria ya Manunuzi, Serikali iboreshe kwa kutoa waraka wa kuangalia value for money pamoja na bei halisi. Maeneo ya kuangalia ni eneo la TEMESA, TBA, Taasisi ya Uchimbaji wa Mabwawa na Visima pamoja na maeneo yote tunapopata huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nashauri maeneo yote ambako Serikali inapata mapato au maduhuli zitozwe kwa njia ya kielektroniki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.