Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa pili wa Hotuba ya Waziri Mkuu ameonesha kero za Muungano na jitihada za kuzitatua. Naomba kuishauri Serikali isishughulikie kero za Zanzibar peke yake, ni vema kukawa na utaratibu wa kuziangalia kero za Tanganyika na iache kuipendelea Zanzibar. Kwa mfano, katika sherehe za Mapinduzi, Dokta Shein hupigiwa mizinga ishirini na moja wakati yeye sio Amiri Jeshi wa Tanzania. Jambo hili linatukera Watanganyika na linamshusha hadhi Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa jambo hili halihitaji mabadiliko ya Katiba, basi Serikali iache kumshauri Rais kuhudhuria sherehe hizo kama tunataka Dkt. Shein ndiye awe mgeni rasmi ili itifaki iweze kuzingatiwa na kama Rais wa Jamhuri atahudhuria, basi yeye ndiye awe mgeni rasmi.