Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona niishauri Serikali kuhusu ng’ombe kupigwa kuchapwa na kuwekewa namba. Jambo hili limesababisha mazao ya ng’ombe kukosa soko kwani ngozi nyingi za Tanzania zimeendelea kukosa soko. Nishauri Serikali kutafuta njia nyingine ya kutambua mifugo badala ya alama hizi kwenye ngozi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Serikali kuongeza juhudi za kuwawezesha wajasiriamali. Kwa mfano, walioamua kufuga nyuki wanapata shida sana ya kupata vifungashio hivyo wanauza asali zao kwa shida sana na kwa hasara. Niishauri Serikali kuwasaidia wajasiriamali hao kupunguziwa bei ya mizinga badala ya mzinga mmoja kuuzwa kwa shilingi elfu themanini, hali hiyo inasababisha ugumu kwao kumudu bei hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Serikali inapotaka kukopesha mikopo kwa wajasiriamali isiache mbali utafutaji wa masoko ya uhakika kuliko ambavyo wajasiriamali wengi wamekuwa wakitengeneza bidhaa kisha kukosa masoko, hali ambayo imesababisha kushindwa kurejesha mikopo hiyo na hivyo kusababisha fedha hiyo kushindwa kwenda kwenye mizunguko ya ukopeshaji kwa wajasiriamali wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Serikali juu ya ulipaji watumishi waliostaafu uwe wa haraka na umakini mkubwa kwani wastaafu wanapata shida sana kulipwa. Wapo waliostaafu tangu mwezi Julai, 2017 mpaka leo hii hawajalipwa. Niiombe Serikali kuliangalia kwani watumishi hao wamekata tamaa na wengine kupata magonjwa ya msongo wa mawazo.