Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja ya Ofisi ya Waziri Mkuu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Dhana ya D by D. Serikali ya Awamu ya Tatu na ya Nne zimetumia mamilioni ya fedha za walipa kodi kugharamia maboresho ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Ugatuzi wa madaraka ni pamoja na kupeleka rasilimali watu wa kutosha na kupeleka rasilimali fedha za kutosha na kuziwezesha Serikali za Mitaa kukusanya kodi katika Halmashauri zao kwa ajili ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano imeua dhana nzima ya D by D kwa kunyang’anya Serikali za Mitaa vyanzo vikubwa vya mapato nazo ni kodi za majengo na kodi za mabango. Kunyang’anywa kwa vyanzo hivi ni kupunguza uwezo wa Serikali za Mitaa kuimarisha na kuboresha huduma za jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kwa Bunge kupitisha sheria ya kuondoa retention kutoka Taasisi za Umma kama TANAPA, Immigration, Polisi na kadhalika ni kupunguza uwezo wa Taasisi hizi kutimiza wajibu wao kwa kutumia vyanzo vya mapato. Uzoefu umeonesha fedha zikishaingizwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali hazirudishwi kabisa au zinarudishwa kidogo kwa taasisi husika. Matokeo yake ni huduma kuzorota.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iangalie upya uamuzi wake kwa sababu Serikali za Awamu ya Tatu na ya nne ziligundua kwamba ili taasisi zifanye vizuri waachiwe kutumia mapato yatokanayo na vyanzo vya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iimarishe jukumu lake la msingi la usimamizi na ufuatiliaji, jukumu ambalo bado Serikali haifanyi vizuri. Serikali inaposhindwa jukumu la usimamizi/ufuatiliaji na tathmini, inaibua solution nyepesi ya kuanzisha utaratibu/taasisi mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kuitazama upya dhana ya D by D na kuimarisha Serikali za Mitaa kama ilivyokusudiwa.