Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na kwa sababu muda mchache napenda kuanza kwa kuunga mkono hoja na napenda kuwafahamisha Mheshimiwa Mwamoto, Mheshimiwa Mchengerwa, Mheshimiwa King na Mheshimiwa Kitandula na wenzenu Simba moja, Mtibwa sifuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno hayo kwa haraka kabisa napenda niende moja kwa moja kwenye ukurasa wa 31 wa hotuba ya Waziri Mkuu kuhusiana na upatikanaji wa mbolea. Kitabu kimeeleza kwamba upatikanaji wa mbolea ni asilimia 64 maana yake ni kwamba asilimia 36 wananchi wetu hawapati mbolea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na tumeona changamoto nyingi za usambazaji wa mbolea. Ninapenda kuishauri Serikali kutokana na changamoto zilizojitokeza mwaka huu hebu ijaribu kuangalia ili wakulima wetu waweze kupata mbolea sio tu kwa bei nafuu, lakini kwa wakati. Inasikitisha sana kuona mkulima wa Isalavanu, kule Itimbo, kule Kitelewasi anapata mbolea ya kupandia mwezi wa pili wakati uandaaji wa mashamba unaanza mwezi wa kumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niiombe Serikali kwa changamoto ambayo wamekutana mwaka huu kwenye usambazaji wa mbolea, hebu wazipitie na kuona kwamba kwa namna gani tutamsaidia mkulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama vile haitoshi tumeona kwenye ukurasa wa 27 unaozungumzia upatikanaji wa chakula tumekuwa na ziada ya chakula tani milioni 2.6. Lakini wale wanunuzi wa chakula NFRA wamenunua tani 26,000 tu za mahindi maana yake ni kwamba mazao yale ambayo ni ziada yameenda wapi? Yamekosa soko, sasa mwananchi huyu mkulima wa Itimbo, wa Bumilainga mbolea tunamcheleweshea lakini anafanya jitihada anazalisha ziada bado tunamzuia kuuza mazao yake. Kwa kweli tunakuwa tunawafanya wakulima kama second citizen katika nchi yetu.

Kwa hiyo, napenda kushauri maana yake Bunge ni kuishauri Serikali hebu iweze kuona upatikanaji wa mbolea kwa wakati, lakini pia kunapokuwa na ziada ya chakula tuwasaidie wananchi hao kupata soko tusifunge kuwazuia kwamba wasiuze nje kama ilivyotokea kwenye mazao ya mahindi tunawakatisha tamaa, muda ni mchache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili naomba sana Mheshimiwa Mama Jenista Mhagama, Kaka yangu Antony Mavunde nadhani ni mdogo wangu kuhusiana na suala zima la uchumi wa viwanda. Ni kweli tunasisitiza na Mheshimiwa Rais na Serikali kwa ujumla imekuwa mstari wa mbele tunamuona Rais amekutana na Jumuiya ya Wafanyabiashara amesikiliza kero zao, ameelekeza Mawaziri wazitatue.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, rai yangu tunapoita wawekezaji na uchumi wa viwanda lazima twende sambasamba na kuangalia walfare ya wafanyakazi wanaofanya kazi katika viwanda hivyo, itakuwa haina maana leo hii kama mimi mfano pale Mafinga tuna wawekezaji lakini unakuta mama anatoka Changarawe anaenda Kinyanambo C kibaruani anatembea almost kilometa sita mpaka tano mpaka saba; mfanyakazi huyu analazimika kuamka saa kumi alfajiri, ana-risk maisha yake anaenda kazini, mshahara mdogo, hakuna NSSF, hakuna matibabu.

Sasa mambo haya nikuombe Mheshimiwa Mavunde kwa sababu ndio unahusika moja kwa moja Kazi, Ajira na Vijana, tembelea Mafinga, toa maelekezo kwa wawekezaji ili kusudi uchumi wa viwanda uende sambasamba na kuangalia walfare ya wafanyakazi, vinginevyo tutaleta viwanda, lakini hali za wananchi wetu zitaendelea kuwa duni itakuwa haina maana kweli Serikali itapata kodi lakini pia lazima wananchi wetu wafurahie uchumi wa viwanda kwa wao kupata kazi ambazo watalipwa vizuri, lakini pia haki zao zitakuwa zinazingatiwa ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia maana muda ni mchache sana naomba niende haraka kwenye point yangu ya mwisho kuhusiana na sekta binafsi. Nimepongeza jitihada za Mheshimiwa Rais lakini mimi naomba na kupendekeza kwa Serikali kwa mikono miwili kabisa baada ya kukutana na wafanyabiashara wale tumeona kabisa concerns zao na tumeona muda ulikuwa ni mchache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza kwa Serikali na naomna Mheshimiwa Rais akiweza akutane pia na sekta kwa sekta mfano sekta mojawapo sekta ya usafirishaji.