Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DEVOTA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia hoja.

Mheshimiwa Spika, nimepitia vizuri kitabu cha hotuba hii ya Waziri Mkuu. Nilitegemea ningeona mambo mengi humu; nilitegemea Waziri Mkuu angetueleza hali halisi ya siasa ya nchi hii kwa wakati huu.

Mheshimiwa Spika, kwa yale ambayo yanaendelea katika nchi hii, ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea katika Taifa hili, kuendelea kunyimwa kwa vyama vya siasa kufanya haki yake ya msingi ya kufanya mikutano; tunaelewa, kazi ya chama chochote cha siasa katika Taifa hili ni kuendelea kutafuta wanachama wapya na kupima afya yake, lakini hivi sasa hali ya siasa iliyoko Tanzania haifananishwi na nchi yoyote ambayo iko katika nchi za Bara la Afrika.

Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa, kwa nini nasema hali ya siasa si nzuri? Ni kwa sababu ya uonezi wa waziwazi na ukandamizaji wa waziwazi. Mfano mzuri tunaouzungumzia hapa ni baadhi ya viongozi wetu wa chama ambao waliwekwa mahabusu wakala Pasaka mahabusu, akiwemo Mwenyekiti wetu wa Kambi ya Upinzani ilhali Mahakama ya Kisutu ilishatoa dhamana, kwa kisingizio kwamba gari ya kupeleka mahabusu ni mbovu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nje ya Mahakama ya Kisutu ukiangalia wakati tunapewa taarifa hizo zilikuwepo defender zaidi ya 30, magari ya washawasha yalikuwemo katika eneo la Kisutu. Unajiuliza, ni magari hayo hayo ya Polisi yameharibika, yameshindwa kuwaleta watuhumiwa Mahakamani, lakini magari hayo hayo yanazunguka Kisutu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ifike mahali tuseme ukweli kwamba Taifa hili tunataka kulipeleka wapi. Mwanzoni niliposikia kwamba upo mkakati kwamba tukiingia madarakani tutahakikisha tumeumaliza upinzani. Nilijua kuumaliza upinzani maana yake ni kufanyia kazi hoja za msingi za upinzani, ni kuhakikisha malalamiko ya upinzani wanayoyatoa dhidi ya wananchi kwa Serikali yanafanyiwa kazi, ndiyo namna ya kuiua upinzani, lakini namna ya kuua upinzani sio hivyo, ndiyo hivi tunavyoviona sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna matamko yanayoendelea. Mimi juzi nimemsikiliza Rais akiwa Arusha. Anawaambia Askari wa Jeshi la Polisi fanyeni mtakavyo, nipo nyuma yenu, nawa- support. Tunajua kazi ya Jeshi la Polisi na amewapongeza kwa jinsi walivyoshughulikia watu kwenye maandamano. Ukiangalia maadamano yale, watu walivyoumizwa wakiwa kama majambazi, watu wameishia kupigwa risasi, wengine wamekufa; sasa kauli za namna hii zinaipeleka wapi Taifa hili? Kwa maneno mepesi ni kwamba ukiwaambia unawa- support kwa maana hiyo waendelee na kazi hiyo ni nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesikiliza wachangiaji wa wiki iliyopita. Kuna mchangiaji mmoja alisema wapinzani wanalalamika, bilioni sita za uchaguzi it’s peanuts! Bilioni sita kwa nchi maskini kama hii ambayo inaishi chini ya dola moja; bilioni sita tunaona ni sawa kwenye uchaguzi?

Mheshimiwa Spika, nilishangaa kwa sababu unaposema hizi bilioni sita za uchaguzi unazungumzia zile za Tume. Hivi umehesabu gharama nyingine ambazo zinaendana na uchaguzi? Umehesabu nauli za wananchi ambao wanatoka maeneo hayo kwa siku 30 wanapanda daladala wanaenda kwenye uchaguzi? Umehesabu Wabunge ambao wanatoka maeneo yao wanaweka mafuta wanakwenda kwenye uchaguzi? Umehesabu gharama…

T A A R I F A . . .

MHE. DEVOTA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, hivi bilioni sita, Mwananyama watu wanalala chini, bilioni sita ingefanya kazi yake, hiyo bilioni sita anayoiona ni ndogo. Bilioni sita hiyo anayoiona ni ndogo ingefanya kazi kubwa sana kuhakikisha kule kwa Manjunju ambako maji yanafurika kila wakati zingesaidia kuleta plan watu wakae vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ziko gharama nyingine zinazotokana na chaguzi hizi. Unapozungumzia hiyo bilioni sita peke yake hujaweka gharama nyingine, misafara mikubwa kuliko hata ya Waziri Mkuu ya Mkuu wa Mkoa, hujaweka misafara ya magari ya washawasha, hujaweka misafara yanayobeba mbwa kwa ajili ya chaguzi. Vile vile hujaweka gharama za watu waliokufa/waliopoteza maisha ambao wamezikwa kwa gharama za Serikali akiwemo yule binti Akwilina.

Mheshimiwa Spika, hujaweka gharama za Katibu wetu wa CHADEMA Hananasif ambaye naye alifariki, zile zote ni gharama. Kwa hiyo, tusiione bilioni sita tu tukaiona, tukifanya tathmini tunaweza tukaona in reality unaweza ukaogopa kuingia kwenye uchaguzi. Nafikiri kungekuwa kuna namna tu mtu akatoka huko, akaingia huku, tukaendelea! (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. DEVOTA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, naomba kwa ajili ya muda niendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeona Waheshimiwa Wabunge wamechangia sana kuhusu ununuzi wa ndege. Hakuna mtu ambaye anasema ununuzi wa ndege ni mbaya, lakini tunachokilalamikia na kukisema siku zote ni gharama za ununuzi wa ndege. Taifa kama hili kununua ndege tatu cash kwa hali ambayo tunayo.

Mheshimiwa Spika, mataifa yaliyoendelea yote hivi sasa yanaanza ku-withdraw kuingia kwenye biashara za ndege kwa sababu biashara ya ndege returns zake si za karibu hivyo. Ni hasara ku-run ndege. Sasa sisi kwa Taifa maskini kama hili tunaenda kununua kwa cash, tungejifunza hata kwa wenzetu Precision na Fastjet ndege zao wamenunuaje. Ukiangalia zote hizo watu wamenunua kwa mikopo, watu wananunua hisa.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, ukiangalia hata huo unafuu wa ndege tunaoambiwa kwamba zimenunuliwa kwa kodi zetu, ukiangalia leo ATCL kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma unazungumzia karibu, lakini saba lakini ukipanda Fastjet kwenda Dar es Salaam – Mbeya na kurudi ni 230,000. Sasa unafuu uko wapi? Tunaweza tukasema kweli tunaunga mkono ununuzi wa ndege?

T A A R I F A . . .

MHE. DEVOTA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, hivi ndege tulizonazo hizi zinatoka nje ya nchi? Hata hivyo, ningeweza nikaelewa kama tumenunua ndege ambayo inatoka hapa inakwenda Marekani, inaleta watalii, wanakuja moja kwa moja hapa. Hivi niulize hata hiyo ndege kutoka Canada mpaka kufika Tanzania ilichukua siku ngapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nizungumze kuhusu suala la Serikali kujinasibu kwamba inakwenda kupambana na ufisadi.

Mheshimiwa Spika, pale Manispaa ya Morogoro iko barabara ambayo imejengwa kutoka Kichangani kwenda Tubuyu ina kilometa nne. Kilometa moja tu imejengwa kwa shilingi bilioni 3.4. Barabara hiyo haina mito, haina kona, haina makorongo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)