Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon Munira Mustafa Khatib

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MUNIRA MUSTAPHA KHATIBU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba yake nzuri ambayo inayoweza kumkomboa mwananchi hasa maskini. (Makofi

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuchangia sehemu ya madawa ya kulevya. Tunashuhudia Waziri Mkuu na Wizar aya Vijana jinsi inavyopambana na masuala ya madawa ya kulevya, lakini suala hili kwa kweli bado ni tatizo moja kubwa sana ndani ya Tanzania. Tunaona Mheshimiwa Waziri, askari wanakamata vijana wadogo wadogo kwa issue ya madawa ya kulevya, tunajisahau kuwa vijana wadogo siyo waingizaji wa madawa ya kulevya. Kuna wafanyabiashara wakubwa, kuna viongozi wakubwa, kuna watu maarufu. Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na mapapa hawa na kuachana na ngedere wadogo hawa ambao wao ni watumiaji lakini tunajisahau kama kuna watu ndiyo waingizaji wa madawa ya kulevya; kwa sababu unamkamata kijana mdogo ambae anatumia tu madawa ya kulevya, ukimkamata bado madawa ya kulevya ndani ya nchi yetu yanaendelea kuingia na watumiaji bado wanaendelea kutumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sober house nashukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu alisema kuna sober houses 22 ambazo tayari zimeanzishwa, lakini sober houses siyo solution ya kusema tunaondoa suala la madawa ya kulevya. Hizi sober house kwanza tukumbuka ni nyumba za watu binafsi, kwa hiyo, business bado inaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa vijana waliopo ndani ya sober house wanasema kwamba wakianza kupona baadhi ya sober house wanapewa tena yale madawa ya kulevya ili waendelee kuwepo ndani ya sober house, kwa sababu kijana mmoja aliyopo ndani ya sober house analipia shilingi 400,000, kijana yule akiondoka ile business imeondoka, kwa hiyo, naiomba Serikali ifumbue macho na kuangalia hizi nyumba za sober house ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kama tunataka tuendelee na sober houses ziwekwe ndani ya mwamvuli wa Serikali, hilo ni jambo la kwanza.

Pili, tunataka vijana hawa ambao tayari wameshaathirika na madawa ya kulevya wachukuliwe wapelekwe hospitali, watibiwe, wapatiwe tiba na watakapopona wapewe mtaji badala ya kuwapeleka sober house zile pesa wapewe mtaji kwa ajili ya kuwaanzishia biashara yao, kwa sababu vijana hawa wanakuwa na changamoto za maisha hawana mtaji wa kuanzishia biashara. Zile pesa vijana hawa wapewe kwa ajili ya kuanzisha biashara na wataweza kuachana na madawa ya kulevya na kufanya biashara zao binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la ajira. Naomba niongee ukweli kwa sababu nitakapoongea ukweli nitakuwa nimemsaidia Mheshimiwa Rais, tusimdanganye Mheshimiwa Rais tukimdanganya bado tutakuwa hatujamsaidia, ili tumsaidie tumwambie ukweli, vijana wamekosa imani na Serikali yao kwa suala la ajira, suala la ajira limekuwa changamoto tuwatafutie vijana ajira ili waweze kutatua mambo yao wawe na imani na Serikali yao. Tusipoangalia vijana hawa wote watakimbilia kwenye madawa ya kulevya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua Serikali kwamba haiwezi kuajiri vijana wote ambao wanamaliza shule, lakini tuangalie njia gani tutafanya ili kuweza kuwasaidia vijana kuweza kujikwamua na maisha. Kwanza tukae na mabenki, tuzungumze nayo, yapunguze urasimu, yaweze kuwapa vijana mkopo wenye riba nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, benki zina urasimu mkubwa kijana kama mimi nisingekuwa Mbunge leo hii nahitaji mkopo naambiwa niende na hati ya nyumba natoa wapi? Naambiwa niende na hati ya shamba natoa wapi? Ni lazima tukae tufikirie ni njia gani ya kumkwamua kijana aweze kujiendeleza katika maisha yake. Kuna miradi ambayo kuwa Mheshimiwa Rais ameianzisha, lakini unashangaa wanatoka vijana kutoka Kenya, Malawi, sijui kutoka wapi ndiyo anakuja kusimamia ajira hizo, tunaiomba Serikali ya Chama cha Mapinduzi ajira hizi zote zisimamiwe na vijana wa Kitanzania, kama miradi ya umeme iliyoanzishwa Rufiji, standard gauge na ujenzi wa viwanja vya ndege ajira hizi zote tunaomba zipate vijana wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu afya ya akina mama; kama mwanamke na kama mzazi nitakuwa sijajitendea haki nisipochangia suala la afya ya akina mama. Tulimuona Naibu Waziri akifungua warsha yake kwa vifungashio vya akina mama na akisema kina mama wachangie shilingi 20,000. Bado kwa mwanamke shilingi 20,000 ambaye ana kipato cha chini ni kubwa sana, kwa nini asiseme vifungaishio hivi viwe bure au aweke shilingi 5000 ambayo anajua mwanamke huyo au mama huyu anaweza kuimiliki kila mwanamke wa kijijini, kila mwanamke maskini anaweza kununua vifunganishio hivi, shilingi 20,000 bado kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu mazingira. Kila siku tunamshuhudia mama yetu Mheshimiwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akienda katika warsha za kuendeleza misitu, tusikate miti hovyo, lakini nikwambie ukweli, miti bado itaendelea kukatwa kwa sababu bei ya gesi bado kubwa sana. Mwananchi wa kawaida huwezi kwenda kumwambia anunue gesi shilingi 50,000 akaacha mkaa shilingi 20,000, miti bado tunayo lakini hatujajua ni jinsi gani ya kuweza kulinda miti yetu. Kwa hiyo, hiyo miti tunayopanda tutashindwa kuilinda kwa sababu sasa hivi hatujui ni jinsi gani ya kuilinda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali yangu isaidie akina mama maskini kwa kuweza kupunguza bei ya gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu asilimia 10 inayotokana na vijana, akina mama na asilimia mbili kwa walemavu. Tukiongea ukweli ndani ya Halmashauri yetu hii pesa haipatikani, naiomba Serikali itafute njia ya kuweza kusimamia Halmashauri hizi ili vijana waweze kupata hizi asilimia nne, wanawake wapate asilimia hizi nne, walemavu wapate hizi asilimia mbili jumla itakuwa ni asilimia
10. Halmashauri itakapotenga hii pesa tutakuwa tumepunguza lile tatizo la kusema ajira kwa vijana, watajua jinsi gani kwa sababu ajira zipo nyingi, kijana anaweza kujiajiri kwenye kilimo, uvuvi, lakini kijana huwezi kumwambia leo hii aende akalime kilimo cha locally au aende akavue uvuvi locally lazima atataka kulima kilimo cha kisasa cha kumwagilia maji, kilimo hicho ili uweze kulima uwe na milioni tano isipungue, sasa hizi asilimia 10 zitakazotolewa na Halmashauri zetu vijana hawa wataweza kujisaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la bandari kidogo tu, bandarini pamekuwa na urasimu mkubwa sana, sisi tunaosafiri kupitia baharini pale ndiyo tunaona. Kijana anasafiri na vitenge doti 10 tu anaambiwa sijui TRA achangie, ushuru wa bandari, hebu tufikirie kijana huyu vitenge 10 atapata faida shilingi ngapi, pesa yote ambayo anachajiwa pale bandarini ndiyo pesa yake yote anayopata faida. Kwa hiyo anakuwa anafanya business as usual.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuangalie tena amechangia Bara anaenda Zanzibar anachangia tena, naomba haya mambo tuyaangalie huu urasimu mdogo wa kuondoka na doti 10 hapa za vitenge, halafu kijana yule akienda Zanzibar anakuwa-charged.

T A A R I F A . . .

MHE. MUNIRA MUSTAFA KHATIBU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea taarifa hiyo tena kwa mikono miwili asilimia mia moja. Hivyo ndivyo ilivyo, tunaomba basi Serikali ikae ifikirie hili suala limekuwa tatizo sana kwa vijana wetu, hawatafika wakati wakaweza kujitegemea wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana, ninaunga mkono hoja asilimia mia moja.