Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze kiujumla Serikali na hususani Waziri Mkuu ambaye amewasilisha hii bajeti pamoja na timu yake Mheshimiwa Jenista na Manaibu Mawaziri kwa kutukuka kwenye kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nianze kwenye eno moja ambalo watu wengi na hasa upande wa pili kule wanaona uwekezaji kwenye miradi ya kimkakati kama ujenzi wa reli, ununuzi wa ndege na kazi nyingine ambazo Serikali ya Chama cha Mapainduzi inafanya, wanaona kwamba mpangilio wa rasilimali haukuwa sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe tu mfano, Wabunge waliopo hapa ndani wengi wamekopa pesa, wamewekeza katika kujenga ma-guest (guest houses), kujenga nyumba za kupangisha, magari, wanafanya biashara ili wapate faida na wafanye shughuli zingine. Kwa hiyo, kwa upande wa Serikali kuweza kununua ndege na kuboresha usafiri wa ndege ndani ya nchi yetu inasaidia na sekta zingine, mojawapo tutapata faida. Ili tuweze kuongeza mapato ya Serikali lazima tuboresha usafiri wa ndege ili na watalii wetu waweze kufika maeneo mbalimbali ya nchi. Kama vile Mkoa wetu wa Katavi tuna Mbuga ya Katavi, Nyanda za Juu Kusini vipo vituo vingi tu lakini tatizo ni miundombinu ya kuwafikisha watalii wetu na wananchi mbalimbali. Pia usafiri wa ndege unasaidia mtu unakuwa in efficiency unakwenda kwa wakati na wengi mnapanda ndege kama vile Fastjet ilivyoingia na kubadilisha mind za watu kwamba usafiri wa ndege si ghali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika masuala ya reli; ukiangalia kwa mfano treni inayotoka Tabora kwenda Mpanda inatumia lita 1000, sasa tukiboresha hii njia na kutumia umeme maana yake gharama za uendeshaji itashuka na matokeo yake nauli zitakuwa nafuu na usafirishaji wa mizigo kwa hiyo itakwenda kukuza uchumi. Kwa hiyo, mnapoona kwamba mikakati ya Serikali inafanyika katika maeneo mbalimbali ni mtambuka na kusaidia sekta zingine na kushusha gharama. Kwa hiyo, ni kazi nzuri ambayo inafanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tunajua chini ya Ofisi ya Waziri MKuu wanashughulika na Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu nitagusa hayo maeneo kama ifuatavyo:-

Ningependa sana niunganishe upande wa kazi pamoja na vijana. Tunajua kabisa asilimia kubwa ya Watanzania ni vijana na wengi wanahitaji kuweza kupata ajira na maeneo mengi kwa mfano Jimbo la Nsimbo asilimia 95 ya wananchi wanashughulika na kilimo. Sasa ningeomba kwa upande wa Serikali tujaribu kuangalia kwenye sekta ambazo zinatoa ajira kubwa upande wa kilimo. Ni jinsi gani tutahusisha kuboresha kilimo katika nyendo zake pamoja na hali ya hewa kwa sababu tunategemea tu mvua moja, sasa namna gani tutalima mara mbili na kuongeza hayo maeneo ili tuendelee kuboresha upande wa ajira.

Mheshimiwa Mwneyekiti, sambamba na kilimo, tunajua kaulimbiu ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika hii Awamu Tano ni kwenda kwenye nchi ya viwanda, sasa malighafi ya viwanda tulivyonavyo inahitaji pia malighafi kutoka upande wa kilimo. Sasa hivi viwandani vinavyohitaji malighafi za upande wa kilimo tunahakikisha kwamba tunafanya nini. Kwa sasa hivi tuna viwanda vingi vinavyotumia malighafi kutoka nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano ukienda kwenye ngano, mafuta ya kula. Tuchukue tu mfano Bakhressa ambaye anatoa ngano na tunapata unga, sasa asilimia kubwa ya malighafi ya Bakhressa inatoka nje ya nchi, sasa kwa kiasi gani tunakwenda kuwavutia wawekezaji upande wa kilimo na kuwashawishi wananchi wetu waweze kulima hizi kwa ajili ya viwanda ambavyo tayari vinatumia malighafi za kutoka nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwa upande wa mafuta ya kula, asilimia kubwa tunaagiza kutoka nje. Ni jinsi gani tutapunguza uagizaji wa mafuta kutoka nje na tuweze kujenga zidia ajira zetu upande wa vijana na wananchi katika Tanzania yetu. Kwa hiyo, tuombe Serikali huu mkakati unakwenda kwa namna gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la upande wa umeme vijijini. Bahati mbaya hatuwezi kuingiliana kwenye kuzungumzia mihimili, lakini naomba tu tuseme Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Kigoma kwa umeme vijijini, Mkandarasi kesi iko mahakamani kila siku inasomwa haijaanza kusikilizwa. Sasa ni lini itakamilika ili wananchi waingie kwenye kupata huduma ya umeme kama ilivyo azma ya Serikali? Kwa hiyo kwa namna nyingine basi na mhimili mwingine uone jinsi gani ya kuharakisha hiyo kesi ili miradi ya maendeleo kwa upande wa umeme vijijini ikatekelezwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tozo mwaka jana tuliibadilishia sheria na tuliweza kutoa tozo na kuweka nafuu chini ya tani moja, lakini tulisahau kwenye bidhaa ambazo hazidumu kwa muda mrefu (perishable goods). Sasa ni jinsi gani utaitoa shambani ukaitunze nyumbani kama vile nyanya, hoho, mboga mboga? Hapa tulipasahau kupaangalia. Sasa tumekuwa nachangamoto kwa wakulima wanakuwa wanatuhoji kutokana na kauli na maelekezo ya Serikali kutokutoza chini ya tani moja unapotoka Halmashauri moja kwenda Halmashauri nyingine.

Mheshimiwa Mwenytkiti, tatizo tulilonalo ni kwenye mboga mboga na bidhaa nyingine ambazo hazidumu (perishable goods). Kwa hiyo, Serikali naomba mliangalie, na nashukuru Mheshimiwa Jafo nimeshamtaarifu na barua nimeshamwandikia, basi lishughulikiwe kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu walemavu; kama Sheria Namba 9 ya mwaka 2010 ilivyo, kuna Mabaraza ya Kata nao wawezeshwe katika ile asilimia 10 ambayo inakwenda kwa vijana, akina mama pamoja na walemavu asilimia mbili. Tuwe na uwezeshaji wa miradi ya moja kwa moja kwa ajili ya kusaidia walemavu ili waweze kujiongezea kipato na waache utegemezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsanye, naunga mkono hoja.