Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Makubaliano ya Paris chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Makubaliano ya Paris chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi nichangie Azimio hili ambalo ni muhimu sana katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Waziri, niipongeze Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kwa taarifa yao nzuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu miaka ya 1960 haikuwa hivi, ilikuwa nchi nzuri sana, ilikuwa na misitu mikubwa na mito ambayo inatiririsha maji mwaka mzima. Kwa sababu ya shughuli za kibinadamu watu wamefyeka miti, wamechoma moto hovyo na mifugo isiyozingatia maeneo ya malisho sasa hivi misitu mingi sana katika maeneo yetu imekwisha. Misitu ndiyo inayoleta mvua na hali ya hewa nzuri na mito ndiyo inayoleta maji.

Maji ni uhai, maji ni maendeleo na maji ni uchumi wa nchi yetu. Lakini vyote hivi uharibifu huu wa ufyekaji, uchomaji moto hovyo ndiyo umesababisha majangwa, umesababisha ukame katika nchi hii kama Kamati ilivyoelezea ukame, milipuko ya magonjwa, viwanda, kemikali hizi, maji machafu yanamwagwa hovyo, madawa, makemikali yanasababisha watu wanapata magonjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, sasa hivi takataka zinachomwa hovyo hata mijini utakuta mtu anachoma takataka sasa zile takataka zinatoa moshi, ule moshi unaharibu hali ya hewa badala ya watu kuvuta oxygen wanavuta carbonmonoxide, kwa hiyo ile ni pollution of air by combustion ambayo inaleta matatizo makubwa sana sana kwa Wananchi wetu wanapata matatizo ya magonjwa ya kifua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hali ya hewa inabadilika kunakuwa na joto kwa sababu ya mabadiliko hayo mpaka wakati fulani unakuta hata bahari maji nayo yanaongezeka. Kwa hiyo, wito wangu kwa kumuunga mkono Mheshimiwa Waziri kwamba wananchi wazingatie kutunza mazingira, bila kutunza mazingira nchi hii ndugu zangu tutakwenda wapi? Maji yatakwisha na bila maji dunia hii tutaishi wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimkushukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kuiweka Wilaya Mpwapwa, naomba nisome kidogo; “Mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya vijijini, Mfumo wa ikolojia na lengo la mradi huu ni kuongezea vijiji uwezo wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi” na Mpwapwa imo. Mpwapwa ilikuwa na misitu mikubwa sana, kulikuwa na Mto Shaban Robert wote mnaufahamu mmesoma kwenye vitabu, Shaban Robert. Ulikuwa unatiririsha maji mwaka mazima, sasa hivi uko wapi? Hakuna, umekauka kwa sababu watu wamechoma, watu wamefyeka hovyo mpaka sasa hakuna na kuna baadhi ya vijiji kuna ukame umeanza, barabara zinaharibika kwa sababu watu wamechoma, watu wamefyeka hovyo kwa hiyo, maji yanakuja kwa kasi yanaharibu barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, naungana kabisa na Mheshimiwa Waziri kwamba azimio hili naliomba Bunge wote tukubaliane liweze kupita bila kupingwa na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.