Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nianze kwa kuipongeza hotuba iliyowasilishwa na Kambi ya Upinzani hapa Bungeni. Kwa bahati mbaya Mheshimiwa Waziri hata leo hayupo na wakati hotuba ile inawasilishwa hakuwepo lakini bahati nzuri kipindi chote Naibu Waziri amekuwepo. Kwa manufaa ya Taifa hili, naomba hiyo hotuba pamoja na kwamba ina kurasa nyingi hebu wajaribuni kuisoma, itawasaidia sana na itasaidia Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujisema mimi mwenyewe kwamba miaka ya 2000 niliwahi kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani ndani ya Bunge hili nikiongoza vyama vitano. Kwa hiyo, bajeti zote ambazo zilipita wakati wa kipindi changu nikiwa Kiongozi (KUB) ni bajeti ambazo hata tukienda kutafuta kwenye Hansard, hakuna bajeti hata moja ambayo Wabunge wa CCM hawakuipitisha mia kwa mia, hakuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia hata nilipokuwa gerezani kwenye kesi feki ya ugaidi kwa kipindi cha miezi kama minne hivi, nampongeza Kamishna wa Magereza aliruhusu nika-own radio nikiwa gerezani na kipindi cha bajeti zilipitishwa kwa maneno matamu kweli na Wabunge wa CCM. Yale maneno haijawahi kutokea, hii ni bajeti ya kihistoria, hii ni bajeti ya kizazi kipya, kwangu mimi ambaye nina experience na Bunge hili chini ya Chama cha Mapinduzi na Serikali yake ni maneno ambayo mimi nayaona ni swaga za kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nadanganya twende tu huko mbele, hakuchi, kutakucha hata hii bajeti utasikia inapigwa mapiku hata bajeti zingine zijazo. Kwa hiyo, kwangu mimi nafikiri mvinyo ni ule ule kinachobadilika ni chupa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Waziri atakapokuja ku-wind up na najua atatanguliwa na baadhi ya Mawaziri ambao wako Serikalini kujibu katika maeneo yao, hebu tuambieni wananchi wa Kagera, Bukoba, Kanda ya Ziwa meli ambayo tumekuwa tunaahidiwa tangu MV Bukoba izame na watu wengine bado wamo humo humo ndani ya meli hiyo mpaka leo, inaonekana wapi katika nyaraka hizi, hotuba hii na bajeti hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wametaja meli za Nyasa, viwanja vya ndege ambavyo vimekuja baada ya tukio la MV Bukoba na hata lugha ya kuizungumziazungumzia hii meli mpya ambayo tumekuwa tunaahidiwa na Awamu zote za uongozi wa nchi hii chini ya Chama cha Mapinduzi inaanza kueleaelea au kufutikafutika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua, badala ya kuelezwa kijuujuu tuelezeni maandalizi ya hiyo meli yako wapi, inakuwa designed wapi, nchi gani na imetengewa hela kutoka wapi? Taarifa hizi zitasaidia wananchi wa Kagera, Bukoba na Kanda ya Ziwa kwa ujumla kufahamu moja nini kinachoendelea. Kama wametupotezea tu kijuujuu ni bora wakatamka bayana kwamba hamna hela na wala hamna nia ya kutupa meli mpya. Sasa hivi dunia ni kijiji, mimi naamini kuna watu wako nchi nyingine wanaweza kujitolea kutuletea meli wananchi wa Kagera, Bukoba ambao wanatambua mateso tunayoyapata kuliko kuendelea kuuziwa mbuzi kwenye gunia (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kahawa, tumesikia hapa kodi zimeondolewa. Nataka Waziri atakapokuja ku- wind up na kwa kuwa nafahamu hata Waziri wa Kilimo anaweza akachangia katika ku-wind up kwa upande wa Serikali atueleze maana sehemu kubwa ya kodi zilizoondolewa zinawazungumzia watu wa kati na wale ma- processor. Watu wa Kagera na Bukoba Town ambao tuna vijiji vinavyolima kahawa pale greenbelt vijiji vya Kata za Kibete, Kitendagulo, Iduganyongo, Nyanga wanauza kahawa, wawaeleze kilo moja kwa kodi hizi zilizopungua inakwenda kupanda kwa kiasi gani? Hicho ndicho mkulima anachohitaji siyo maneno maneno haya ya jumla jumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, nakubaliana na nawaunga mkono Waheshimiwa Wabunge waliochangia sana hapa kwamba katika suala la madini na vita ya rasilimali inayoendelea inahitaji uzalendo na mshikamano wetu wote. Hilo naliunga mkono na naweza nikalipigania mimi kama Lwakatare. Hata hivyo, uzalendo ni lazima utengenezewe mazingira. Huwezi kutoka hewani unazungumzia tuwe wazalendo, tuwe na mshikamano, lazima tutengeneze mazingira ambayo yatawezesha, kwanza tuheshimiane humu ndani, tutambuane umuhimu na tuheshimu hoja ambazo ni kinzani kwa nia ya kujifunza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi binafsi maana natoka Kagera mimi Mlangira mimi, sili chakula ambacho ni half cooked, ni kwamba mambo ya kubebeshana maiti ambapo hatujui marehemu kafia wapi tunakuja kubebeshana tu, mimi siko tayari kuibeba hiyo maiti. Tungetaka kutokea kwa viongozi wetu wakuu wawe consistency maana kiongozi anakwenda mahali fulani anasema mimi kwa capacity yangu siwezi kumteua Mpinzani kwenye Serikali yangu, haijapita kipindi anateua Wapinzani. Jamani dunia ni kijiji kuna wenzetu wanatushangaa kwa matamko tunayoyatoa. Hiyo inafanya tunashindwa kuwa na consistency ya matamko ya viongozi wetu na dunia wanashindwa kuelewa. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ninalotaka kumalizia nalo, naomba bajeti hii Mheshimiwa Waziri leo yuko Naibu Waziri lakini Serikali iko pale pale, wamwongezee pesa Msajili wa Vyama vya Siasa na iende purposely kwa ajili ya kujenga capacity kwenye vyama vyetu, vyama vinapaswa kujengewa capacity. Chama cha kwanza ambacho kwa kweli kutokana na michango na yale yanayoendelea naona kijengewe capacity ni Chama cha Mapinduzi. Haiwezekani kwa miaka 56 ya Uhuru tunaendesha Serikali kwa individual capacity badala ya taasisi. Matokeo yake Mheshimiwa Rais wamemuachia mzigo ndiye anaendesha Serikali wakati tuna Baraza la Mawaziri hewa, viongozi wa taasisi hewa, Wakurugenzi hewa kwa sababu wote wanakwenda kwa mtindo wa ndiyo mzee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani yanayoonekana sasa hivi na mimi namkubalia Ndugu yangu Mheshimiwa Bwege alisema sasa hivi inayoendesha Serikali ni Serikali ya Magufuli aliyoisema yeye mwenyewe, Watanzania chagueni Serikali ya Magufuli, hakuna Serikali ya CCM hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo ya hili inazaa suala la watu kujipendekeza, kila mmoja anajipendekeza kwa mtu mmoja anayeendesha Serikali. Msajili akijengee Chama cha Mapinduzi capacity ya kuendesha Serikali kitaasisi. Matokeo yake huyu Rais jamani tutamuua bure, kubeba mizigo ya Wizara zote, taasisi zote, makontena ya madini anatembelea yeye, yeye ndiyo anapanga bajeti, akiamua sijuiā€¦ (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)