Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nami kwa kupata nafasi. Napenda kuipongeza Wizara ya Fedha na Mipango kwa jinsi ambavyo tulishirikiana wakati watu wa Halmashauri wa Mji wa Mafinga tulipopata msaada kutoka Ubalozi wa Japan. Kulikuwa na some complications, lakini kwa ushirikiano mkubwa tuliweza kufanikiwa kiasi kwamba tukafanikiwa kupata huo msaada baada ya Wizara kufanya marekebisho ya kanuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nichangie katika bajeti hii kwa kuanza kusema yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema ni wizi katika Sekta ya Madini, nilikuwa najaribu kupitia nyaraka mbalimbali, mojawapo, ni hii inasema protecting your community against mining companies. Katika document hii imeeleza kwa ufasaha namna gani makampuni makubwa ya madini yanavyofanya mbinu mbalimbali ambayo hitimisho lake ndiyo tunaita wizi. Katika utangulizi wa document hii anasema:

“The company may deliberately try to disrupt and weaken a community’s ability to organize effectively against them.” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maana yake ni nini? makampuni yanaweza yakatumia mbinu mbalimbali yakatugawa sisi ili tusiweze kushikamana katika kukabiliana na wizi mbalimbali ambao wanaufanya. Wizi huu unafanyikaje? Kwa sababu wenzetu wako mbali kwa teknolojia na mbinu mbalimbali za kufanya international trading. Moja, wanafanya kitu tunaita trade mispricing. Ndiyo ile wakileta machinery wanakuza bei baadaye wanadai tax refund. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine, wanafanya kitu kinaitwa payment between parent companies and their subsidiaries, ndiyo maana tulikuwa tunagombana na Acacia lakini amekuja kuibuka Mwenyekiti wa Barrick ambayo ndiyo Kampuni Kuu. Pia wanafanya wizi huo kwa kutumia profit shifting mechanism ambayo imekuwa designed ku-hide revenue, ndiyo maana tunaita wizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, watatumia mbinu nyingi kutu-divide. Gazeti la The East African la wiki hii limeandika, “Magufuli Fight for Mineral Revenue Splits Parliament.” Hiki siyo kitu kizuri kwetu kama Taifa. Lazima sisi tubaki kitu kama kimoja. Kama Bunge, kama Taifa, lazima tuwe nyuma ya Mheshimiwa Rais ambaye ameamua kuthubutu kukabiliana na huu wizi mkubwa wa Kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Director wa Global Justice anasema kuwa Afrika siyo maskini na ukipitia ripoti mbalimbali za Taasisi za Kimataifa, zinasema kwamba kupitia makampuni haya, fedha inayoondoka ni zaidi ya mara kumi ya fedha wanayotupa sisi kama misaada. Maana yake ni nini? Ukienda kwenye bajeti yetu, karibu shilingi trilioni saba ni mikopo, misaada na fedha kutoka kwa wahisani; lakini inayoondoka kupitia wizi huu niliousema, maana yake ni mara kumi ya shilingi trilioni saba. Kwa hiyo, zinazoondoka hapa nchini kwetu ni shilingi trilioni 70, ndiyo maana tunasema wizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa hizi zinazoondoka kwa mbinu hizi mbalimbali ambazo Mheshimiwa Rais ameamua kuwa na uthubutu ili tuweze kukabiliana na multinational companies, lazima sisi kama Taifa na kama Bunge tuwe united, tusigawanyike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais kwa nini ameweza kuwa na uthubutu? Ukisoma gazeti la Sunday Nation la Jumapili linasema, “Uhuru tycoons raise millions in two hours” kwa ajili ya kampeni, lakini we are lucky Rais wetu ameingia pale hakuwa na backing ya watu wenye hela chafu, kwa hiyo, tunapopata kiongozi wa namna hii, lazima tuwe united kumuunga mkono, kwa sababu tunachozungumzia ni upotevu wa mapato ambayo yakipatikana wote tutafaidika. Wote hapa tunalia, nami nalia kuhusu kukosekana maji, umeme, huduma bora za afya, kuanzia Lumwago, Bumilanyinga, Isalavanu mpaka Itimbo na Mafinga kwa ujumla. Sasa anapotokea kiongozi mwenye uthubutu ni lazima sisi tushikamane kumuunga mkono kukabiliana na multinational companies. Haya madude ni hatari sana, nitawaambia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hugo Chaves alipoingia madarakani tarehe 11 Aprili, 2002, alifurumua mikataba kama anavyojaribu kufanya Mheshimiwa Rais. Madude haya (multinational companies) yaliji-organise yakafanya hujuma kumwondoa madarakani lakini kwa sababu Bunge na wananchi wa Venezuela walikuwa united, baada ya masaa 47 alirudi Ofisini. Ndiyo maana nasisitiza ndugu zangu tuwe kitu kimoja kukabiliana na madude haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu siyo wakati wa kutafuta personal recognition. Kila mtu kwa nafasi yake alipaza sauti kuhusiana na hujuma na wizi huu. Wapo waliokuwa wanaharakati wakati huo kama Mheshimiwa Tundu Lissu, wapo waliokuwa Wabunge kama Mheshimiwa Peter Serukamba na Mheshimiwa Kigwangalla ametajwa hapa, wapo akina Rugemeleza na Nshema wale wa LEAT wote walipaza sauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mwaka 2008 Mawaziri wanaohusika na Sekta ya Madini walikutana kujadili katika Afrika namna gani tutanufaika kutokana na madini. AU Summit 2009 ilipitisha azimio ni kwa namna gani tutaendelea kunufaika na madini na kuachana na wizi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2011 Mawaziri wa madini katika Afrika walikutana na kujadili na kuja kitu kinaitwa “From Mission to Vision”; na hiki ndicho Mheshimiwa Rais anachofanya. Ametoka from mission to vision to action. Sasa ameingia kwenye action. Anapoingia kwenye action, sisi tuna kila sababu ya kumuunga mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitaka ujue wizi huu, nenda kasome kitabu hiki cha Nicolaus Shakson; (Treasure Island), “Uncovering the Damage of Offshore Banking and Tax Havens.” Yote haya ni wizi unatumika. Vile vile kasome kitabu cha Mwandishi the same; “Poisoned Worse; The Dirty Politics of African Oil.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, nenda kaangalie document inaitwa “Stealing Africa.” Why is Africa so rich in resources, yet so poor? Ni kwa sababu ya wizi wa namna hii ambao lazima tukubaliane tuwe united kama Taifa, tuwe pamoja kama Bunge na kwa maana hiyo, tutaweza sana kufanikiwa. Vinginevyo tukitafuta muda wa recognition, kila mtu played his/her own part. Viongozi wa dini walisema, wananchi wa kawaida walisema, wanaharakati walisema, Wabunge walisema. Kwa hiyo, ni wakati ambao tunatakiwa tukwepe sana kugawanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia, wakati anaapishwa Commisioner wa TRA, Mheshimiwa Makamu wa Rais alisema, “Maafisa wako na Mameneja wa Mikoa waache kutoa kauli za kuigombanisha Serikali na wafanyabiashara, wakusanye kodi kwa kufuata sheria na taratibu na pia wawe na lugha nzuri.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu kinaitwa Mawakala wa TRA, lugha yao na operation namna wanafanya, ni kuigombanisha Serikali na wananchi. Naiomba TRA, pamoja na kutoa elimu ya mlipa kodi, ijaribu kukaa na hawa Mawakala wao iwe inawapa hata training ya namna gani ya kufanya customer care. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu muda umeniishia naona unanikimbia; katika makinikia haya, yako mengi. Sisi kule Mufindi suala la misitu, nimeshaandika hata katika mchango wangu; MPM wanauziwa magogo mpaka leo nusu ya bei pasipo sababu. Hayo nayo ni makinikia. Kwa hiyo, naiomba Serikali, kama ilivyoanza katika dhahabu, kuna makinikia kwenye misitu, kuna makinikia kwenye fishing industry kutoka bahari kuu, kuna makinikia kwenye mambo mengi, hata kwenye mchezo wetu wa soka kuna makinikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.