Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nami nichangie machache katika bajeti ya Serikali ambayo ipo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, Wabunge tunapokaa katika ukumbi huu kazi yetu ni kuisimamia na kuishauri Serikali, lakini kwa bajeti hii ambayo iko mbele yetu ni vizuri Serikali ikawa wazi ili tuishauri na tuisimamie. Hata hivyo, kama mtaleta vitu kwa mafungu na bila kufanya analysis ya kina maana yake hamtupi nafasi ya kuwashauri ili mfanye vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti hii ambayo tunaitumia sasa ni wazi kwamba Serikali imefikia malengo kwa asilimia 70 ya makusanyo, lakini kwenye makusanyo hayo ambayo mlikuwa mnategemea trilioni 29, trilioni 11 mmekusanya ya kodi lakini leo mnaleta trilioni 31 wakati makusanyo yetu yako asilimia 70. Mngetuambia tu ukweli, kwamba ni wapi mmekwama? Kwa sababu gani na mnarekebishaje? Kwa haya mnayotuletea kwamba kila mwaka mnakuza bajeti ambayo haitekelezeki mnawadanganya Watanzania siyo kweli. Ni bora mseme ni wapi mmekwama na tuishi according to bajeti ambayo tunaweza tukakusanya na tukapeleka kwenye miradi ya maendeleo, lakini kama mnataka tufanye biashara kama biashara mtapitisha bajeti hii lakini utekelezaji haupo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nalisema hili kwa sababu ni bahati mbaya sana leo Serikali mnawaza kuzimisha kabisa Serikali za Mitaa. Makusanyo yenu yote mmekusanya huko mmeshindwa, mnakwenda kuchukua vyanzo vya Halmashauri zetu sasa ni kitu kinachosikitisha na nilishawahi kusema kwenye Bunge hili. Mwaka 1980 Baba wa Taifa alijuta suala zima la kufuta Serikali za Mitaa na kuondoa nguvu za Serikali za Mitaa. Wakati huo barabara zilikwama, zahanati zetu zilikwama kwa sababu fedha zilikuwa haziendi baada ya Serikali Kuu kukusanya. Hii bajeti mnayotuletea leo ni ya kuua Serikali zetu za Mitaa kwa asilimia mia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nalisema hili mwaka jana mlitufukuza hapa mkapitisha bajeti, lakini mkaondoa chanzo cha kodi ya majengo. Mpaka hivi tunavyoongea mpaka leo Serikali haijakusanya, TRA haijakusanya kodi ya majengo ni bora mngetuachia Halmashauri tukakusanya. Kama hilo halikutosha hamkufanya tathmini ndiyo maana nasema mnaleta bajeti kama biashara tu kwamba muda wa kuleta bajeti umefika mnaleta bajeti hamjafanya tathmini. Leo Serikali mngekiri tu kwamba mlishindwa kukusanya na mlifanya maamuzi mabaya kuondoa chanzo hiki katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hilo haitoshi kodi ya ardhi mmechukua, kodi ya mabango mmechukua, uko kwenye minada mmefuta. Naomba Waziri wa Fedha aniambie ukweli wakati anajibu hivi wana mpango gani na Halmashauri zetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyoongea mimi Halmashauri ya Mji wa Babati, nitoe tu mfano, wametuachia vyanzo viwili tu, ushuru wa soko na ushuru wa stendi. Wakati huohuo wanasema kwamba, Halmashauri zetu tuorodheshe idadi ya wazee, tuwalipie bima ya afya, wauna watu tunawalipa mishahara madereva na ma-secretary pale wasaidizi zile kada ambazo Halmashauri zetu zinaajiri, lakini hakuna chanzo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati mbaya sana hizi fedha tunazoambiwa kwamba, leo naomba tu nichangie hii sehemu ya Serikali za Mitaa. Hizi fedha ambazo Serikali mnasema mtakusanya mtatuletea ni uwongo mtupu. Ninavyoongea hivi Mheshimiwa Waziri wa Fedha, nilikwenda nikamwona pale kwenye Kiti nikamweleza hata OC hawatuletei kwenye Halmashauri zetu, hivi ninavyoongea tangu bajeti hii imeanza ya trilioni 29 Halmashauri ya Mji wa Babati wametuletea OC ya milioni 26 tena ya mitihani! Hela ya Walimu wanaoenda kusimamia mitihani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Halmashauri ukienda watu wanaandamana hakuna fedha, hatuna makusanyo, fedha zote wamechukua. Ile asilimia 30 ya kodi ya ardhi ambayo tunakusanya hata hawarudishi tena kwa Wizara ya Ardhi hawatuletei tena! Halafu wao watu wa Mungu binadamu wanasema kwamba, kila kitu kifanyike kwenye Halmashauri, miradi ya maendeleo hawaleti fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele cha Mheshimiwa Waziri kwenye hiki kitabu, fedha zote wamepeleka zaidi ya milioni 500 kwa Jeshi. OC wanazopeleka ni za Jeshi, Polisi, ndiyo hela wanazolipa, lakini huku hawapeleki! Hakuna hela ambazo wanatuletea, leo tutawaaminije kwamba, wao tukiwaachia hivi vyanzo wataturudishia kwenye halmashari zetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu wajitafakari, ni bora wakaacha Halmashauri zikakusanya kwa sababu, wao vipaumbele vyao ni tofauti na walivyoviahidi. Kwenye Uchaguzi Mkuu wakaja wakatuahidi wakasema milioni 50 kwa kila kijiji, hakuna chochote huku Mheshimiwa Waziri. Tena hajaongelea chochote! Mwaka jana wakatenga mikoa sijui mingapi kama bilioni 59, hawakupeleka kabisa hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekaa Wabunge tunaulizwa, Serikali imeahidi milioni 50 kwa kila kijiji ziko wapi? Hata kuzisema tu wamekwepa, hata kuziandika tu, mwaka jana walithubutu kuandika, mwaka huu hawajathubutu hata kuandika kutaja. Wanavyoviahidi tofauti na wanavyotekeleza! Ni nini kinawaroga? Ni nini kinawasahaulisha? Ni kitu gani ambacho kinawafanya wasifikirie waliyoyaahidi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri zetu wametuachia kitu cha ajabu sana, wamepandisha faini za mtu ambaye ametupa takataka, labda kimfuko cha malboro amekidondosha chini, kutoka Sh.50,000/=, wamepandisha mpaka Sh.200,000/= mpaka Sh.1,000,000/=! Eti ndio chanzo wanachotuachia Halmashauri. Ni aibu kwa Serikali ambayo inawaza eti fine ndiyo iendeshe Halmashauri. Yaani wamepandisha eti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ile ni By Laws ya Halmashauri zetu, to be honest, tuwe wa kweli, wala hakiwahusu hicho chanzo, halafu Serikali wanakaa wanafikiria, halafu kingine, ada ya uchafu unapozolewa sokoni wamefuta, hata kuzoa uchafu hawataki tu-charge. Halafu wanaweka faini kwa kitu gani, wakati hata hizo ada za kuondoa tu huo uchafu wameondoa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana nasema wakae wafikirie. Waheshimiwa Wabunge kila mmoja hapa ana Halmashauri yake, Wabunge wa Majimbo, Wabunge wa Viti Maalum tunaingia, hii bajeti wale wanaosema ni bajeti ya karne, wanajidanganya na watapiga makofi watapitisha, lakini kwa upande wa Halmashauri, Serikali Kuu imeamua kunyonga Halmashauri zetu, kuchukua vyanzo vyote, wanatuachia eti tukakimbizane na wananchi, mtu ametoka hospitali kawekewa drip ameenda haja ndogo hapo tukam- charge laki mbili! Nani anaweza kufanya hayo? Hatuwezi kufanya hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri akae chini afikirie, ushauri wangu kwa Serikali na kwa bajeti hii, wakae chini wafikirie warudishe vyanzo vyote vya Halmashauri, ili tuwasaidie kufanya maendeleo kwa sababu barabara zetu hazipitiki, tunavyoongea hatuwezi kuchonga hizo barabara wala kukarabati. Tulishauri katika Bunge hili kwamba, asilimia 70 wanazopeleka TANROAD wapeleke kwenye Halmashauri, 30 iwe viceversa kwa sababu barabara

nyingi za mikoa wameshaunganisha kwa lami. Sasa hivi waturudishie hivyo vyanzo, wabadilishe, hawakutaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kinachotokea sasa kwa sababu wameona kwamba, hawakusanyi huku juu mambo hayaendi, wakaunda task force ile ya TRA ambayo wameweka Usalama wa Taifa, wameweka Polisi huko wanakimbizana na madeni ya nyuma huko, wakati walisema hawatafufua makaburi, leo wanafufua makaburi! Wanaenda wanadai kodi ya 2011 hata wao hawakuwepo kwenye hizo nafasi! (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)