Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata fursa hii ya kuweza kuchangia mjadala huu wa mapendekezo ya bajeti. Nami moja kwa moja napenda nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Waziri wetu Dkt. Mpango, lakini pia napenda nichukue fursa hii kumshukuru Naibu wake na timu nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, popo hajafahamika kama ni mnyama ama ni ndege mpaka hivi leo. Hawa wenzetu hata sitaki kuwaita ni vinyonga, naomba niwaite popo. Maana yake hawajafahamika either ni ndege ama ni wanyama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo limewashuka! Walijigeuza kuwa ni Mawakili wa wale ambao sisi tumewatuhumu kwamba ni wezi wetu na yule mhusika mkuu amewathibitishia mchana wa leo, ameingia na amekiri mwenyewe kwa kinywa chake kwamba wako tayari kulipa pesa tunazotaka au tunazowadai. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tena lile liliokuwa linaonekana kwamba ni jambo gumu la kujenga smelter katika nchi hii amelichukua na amesema wako tayari kujenga smelter katika nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Afrika, our home land; Afrika ina bahati mbaya, Wapinzani wa Afrika wamekuwa wakitumika na mabeberu miaka yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, UNITA wametumika na mabeberu kuiangamiza Angola miaka yote, wale pia wanatumika na mabeberu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna kila sababu ya kutamba. Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, eneo la madini ukurasa wa 32 Kifungu cha 35 (a) kinaeleza wazi wazi, “kuweka na kusimamia mfumo thabiti wa kukagua shughuli za migodi.” Ukienda ukurasa wa 34, hiyo hiyo 35(k) utaambiwa…. (Makofi)

TAARIFA . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaliyotokea mchana wa leo hayawezi kupita hivi hivi, lazima kuna watu wahangaike. Yale mambo siyo mchezo mchezo! Wale Wazungu wakimwaga mzigo hata wa trilioni 10, 20 au 50 tu hapa, haya mambo tunayoyazungumza juu ya barabara zetu, juu ya maji, juu ya shilingi milioni 50 katika vijiji, juu ya SGR, juu ya kuongeza ndege nyingine, juu ya maendeleo yote katika nchi hii, tutapaa! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nikwambie tu na Bunge hili pia, Word Bank wametoa ripoti na wame-predict Tanzania is going to be the third fastest growing economy katika Afrika. Itapitwa na Ethopia kwa 8.3 percent; itapitwa na Ghana kwa 7.8 percent; sisi tutakuwa 7.2. Hiyo ndiyo habari. Nataka nikwambie, ukitaka kuyaona hayo, ndiyo maana utaona watu wamekimbia siti zao leo, wametoka mbele wamehamia kule nyuma. Aibu! Eeh, habari hii ni ngumu! Hii habari ni nzito!

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Dkt. Mpango na timu yake msumari huo umeingia! Hatari sana haya mambo! Huyu JPM sio mtu wa mchezo mchezo, watu wanaweweseka, watu wamepoteza uelekeo! Haya mambo siyo ya mchezo mchezo! (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudi sasa katika bajeti yetu, natoa ushauri ili yale mapato yaendelee kutuimarisha katika uchumi wetu. Dozi imeshaingia, hela za Morena zimepotea, basi tunasonga mbele. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudi katika blue economy. Nasisitiza ya kwamba fisheries, kama Ilani yetu inavyoeleza, tunayo nafasi kubwa sana ya kuendelea kukuza kipato chetu kwa kutumia Sekta ya Uvuvi wa Bahari Kuu, tununue meli tuhakikishe kwamba tunachakata na kufanya maendeleo mengine katika Bahari Kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nichukue nafasi hii pia kuelezea juu ya kilimo. Wapo watu hapa wamesema Serikali hii haishughuliki na kilimo wakija kwetu sisi tunaolima korosho tunaweza tukawapopoa kwa mawe. Sisi tumeambiwa msimu huu wa kilimo, korosho tutapata sulphur bure, mabomba ya kupulizia bure. Ni nani huyo anayeweza kusimama hapa; Serikali imetuondolea zaidi ya tozo tano za kilimo, wewe leo unasimama unasema mambo yasiyokuwa na kichwa wala miguu!

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoomba sasa, sisi kama Taifa tunapoteza siyo chini ya Dola milioni 110 kwa kupeleka korosho ghafi nje ya nchi. Hiyo tukibaki nayo, tunao uwezo wa kutengeneza kiwanda cha kuchakata korosho na tukaweza kuuza na tukatoa ajira za kutosha. Tuweke mkakati maalum kabisa; ule uliowekwa na Bodi ya Korosho wa kuhakikisha tunatengeneza viwanda vyetu, basi hilo tusiliache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kupoteza wakati, katika bajeti hii nimeona mambo mengi; mojawapo ya jambo nililoliona ni misamaha mbalimbali kwa viwanda vyetu vya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.