Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Zainabu Mussa Bakar

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa dunia kwa kuweza kunifikisha katika hali ya uzima katika Bunge hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nawashukuru Viongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani kwa kufanya kazi kwa hali ambayo ni ngumu sana. Jambo la tatu, kabla sijaendelea kuchangia, naunga mkono maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba hii ya Waziri Mpango ambayo ni hotuba ya Serikali, nimeshangaa kwamba hotuba nimesoma yote, lakini halijazungumziwa suala la ajira. Suala la ajira ni suala muhimu kwa kila Mtanzania. Tunaona watu wanamaliza Vyuo mamia kwa mamia, lakini mwisho wa siku wanaranda na vyeti vyao mifukoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama Serikali hii inawapenda Watanzania ni bora wachukue suala hili walifanyie kazi vizuri sana. Kwa sababu suala la ajira ni muhimu kila mtu anapatia mahitaji yake. Nasema hivi kwa sababu wananchi wa Tanzania hawajapewa elimu ambayo
itawawezesha kujiajiri. Pindi watapewa elimu ya kujiajiri ndiyo hili suala ambalo pengine lingeweza kufanywa, kwa hivi lilivyofanywa katika bajeti hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nataka kulizungumzia ni suala la kilimo; Kilimo ni uti wa mgongo. Marais mbalimbali walikuja na kauli mbiu mbalimbali. Kuna wengine ambao walisema Kilimo kwanza, lakini naona katika bajeti hii haijapewa kipaumbele. Kilimo kimedharauliwa, ukiangalia kwamba kilimo chetu kinakuwa kwa asilimia 1.7, hii ni kwamba Serikali hii ya CCM haijakipa kilimo kipaumbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo kilitarajia kifikie asilimia sita ya kukua lakini mpaka sasa hivi kilimo kimefikia asilimia 1.7. Hii ni ndoto kwamba tutategemea Serikali ya Viwanda, Serikali ya Viwanda itakuwa haipo kwa sababu kilimo hakijapewa kipaumbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nakusudia kulizungumza ni kwamba Serikali hii katika bajeti yake Mheshimiwa Waziri Mpango, haijatuambia kwamba imetekeleza kupunguza umaskini kwa kiasi gani? Nimesoma bajeti hii lakini sijaona sehemu ambayo Serikali kama imejipanga na kama iko tayari kuwasaidia Watanzania kutuambia kwamba wamejipanga ni namna gani watapunguza umaskini Tanzania? Tunawaona akinamama na akinababa wanaangamia kutokana na kwamba umasikini umekithiri katika nchi hii ya Tanzania. Tukizungumzia umaskini ni kwamba, katika maeneo mengi wananchi wa Tanzania wako katika hali duni. Kwa hiyo, ni muhimu sana bajeti hii ilikuwa ielezee ni kiasi gani itapunguza umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la Motor Vehicle. Katika bajeti hii tukiangalia ukurasa wa 48, tumeambiwa kwamba watu ambao wana magari wamesamehewa ada ya kulipa Motor Vehicle. Kiukweli ni kwamba ada hii haikutolewa bali imepelekwa kwenye vyanzo vingine. Ni jambo ambalo linawaumiza Watanzania hususan watu ambao wanaishi vijijini. Tozo hii imewekwa katika mafuta ya taa Sh.40/=. Hii inamkandamiza mwanamke wa kijijini, inawakandamiza wananchi wote wa vijijini kwa sababu wao ni watu wa hali duni, kuwalipia watu wenye wanamaslahi makubwa, watu wa kati na wakubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tukisema kwamba hatujamkandamiza Mtanzania ambaye yuko katika hali ya chini, hii itakuwa siyo kweli kwa sababu bajeti yetu imeonesha kwamba inawapendelea sana watu wa kati na matajiri kuliko watu wa chini. Kwa hiyo, naiomba Serikali, kama ikiwezekana, ada hii kama hawataki waiweke katika Motor Vehicle, basi waifute kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nitakalozungumzia ni kuhusu madini. Madini ni Rasilimali muhimu katika Tanzania hii. Ni jambo la kushangaza kwamba madini yetu yanaibiwa kila siku kwa sheria za ovyo ambazo zimetungwa na Serikali ya CCM. Leo hii wanakaa hadharani kutaka kujisafisha jambo ambalo haliwezekani. Ni bora kwanza waseme ukweli kwa sababu kulikuwa na Waheshimiwa Wabunge wengi wa Kambi Rasmi ya Upinzani wakilizungumzia suala hili, lakini mkiwaona sio lolote sio chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii Tanzania imeshaibiwa matrilioni kwa matrilioni ndiyo leo tunaona kwamba mtu au Kiongozi anatoka hewani na kusema kwamba tunaibiwa. Tumeibiwa sana na tutaendelea kuibiwa kama hatutarekebisha mikataba yetu na sheria zetu. Nasema hivyo kwa sababu gani? Tuna madini pia ya Tanzanite ambayo Tanzania pekee ndiyo ambayo…

TAARIFA . . .

MHE. ZAINAB MUSSA BAKARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza taarifa hiyo siipokei, kwa sababu mimi sikumtaja kama ni Mheshimiwa Rais. Kama umejishuku itakuwa ndio huyo huyo. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kuchangia katika maoni yangu ni kwamba Tanzania hii ni pekee ambayo inazalisha Tanzanite, lakini leo kama hatuibiwi, Tanzania ni nchi ya nne ambayo inauza Tanzanite. Hivi nchi nyingine madini haya wanapata wapi kama itakuwa hatuibiwi? La muhimu ni kukaa tukaweza kurekebisha sheria zetu, zikaletwa hapa ili tuondoe janga hili la kuibiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuzungumza, ni kwamba… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)